Vipimo
Vikombe Vinne (4) Vya Unga Wa Ngano Mweupe
Vijiko vi tatu vya samli
~vijiko viwili vya chumvi
vikombe viwili vya maji ya uvugu vugu
samli (mafuta) ya kupikia chapati
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Mimina unga, samli na chumvi kwenye sinia au bakuli kubwa. Changanya pamoja.
- Mimina maji kidogo kidogo huku unachanganya na ule mchanganyiko wa unga.
- Mchanganyiko ukishashikana, kanda unga kwa mkono kiasi, kama dakika tano hivi.
- Finika na uache mchanganyiko kwenye sinia kama dakika kumi hivi kwa kuufunika ili hewa isiingie.
- Gawanya ule mchanganyiko kwa kufanya madonge kama kumi na nne au kumi na sita kwa chapati ndogo.
- Mimina unga kidogo mahali ambapo utasukuma chapati.
- Sukuma donge moja mpaka liwe duwara jembamba.
- Paka samli kama kijiko kimoja cha kulia, ukihakikisha umepaka duwara lote.
- Kunja lile duwara kama mfano wa kamba, huku unazungusha kama kamba ili iwe ndefu kidogo.
- Zungusha ile kamba iwe mviringo. Funika na kitambaa kisafi cha jikoni ambacho kimajimaji kidogo.
- Endelea namna hii mpaka umalize madonge yote.
- Sukuma chapati iwe mviringo kama nchi 7 hivi
- Pika chapati kwenye frying pan moto wa kiasi. Ikiiva upande mmoja na kuanza kufura, geuza upande wa pili. Tumia kitambaa kisafi cha jikoni kupress na kuzungusha zungusha ile chapati. Ikiiva upande wa pili, mimina kijiko kimoja cha kulia cha samli na ugeuze chapati tena, zungusha zungusha kisha mimina nusu kijiko cha kulia cha samli na ugeuze upande wa pili kidogo. Toa chapati uweke kwenye sahani. Ikunje kunje kidogo kisha uifingue vizuri.
- Endelea namna hii huku unafuta frying pan na kitambaa kisafi au karatasi za jikoni (tissue) baada ya kila chapatti.
Kidokezo
Unapomaliza kuzipika kila moja, zitandaze kwanza chapati katika sahani (au sinia) kubwa zipate kupoa ziwe kavu ili zisinyonyanye mafuta. Kisha tena ziweke katika sahani yako ya kawaida.
Unaweza ku freeze chapati katika Freezer bags. Kunja chapati moja moja ziwe nusu. Zifunike na Wax paper, kisha zitie kwenye freezer bags na uzihifadhi katika freezer. Unapotaka kula, toa kwenye freezer na upashe moto katika Microwave.
MCHUZI WA KUKU
mahitaji:
Chicken marination:-
Kuku mzima
Chumvi kjk 1 cha chai
Mtindi vjk 2 vya chakula
Binzari ya manjano 1/2 kijiko cha chai
Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai
Ndimu 1
Vitunguu saumu 1/2 kjk cha chai
Tangawizi 1/2 kjk cha chai
Filling
Biringanyi 2
Viazi 2
Kitunguu maji 1
Nyanya 2
Hoho 2
Binzari nyembamba ya unga 1/2 kjk cha chai
Giligilani ya unga 1/2 kjk cha chai
Chumvi
Garam masala 1/2 kjk cha chai
Maandalizi:
Chukua mahitaji yote ya marination changanya pamoja kisha pakaza kwenye kuku kwa juu na ndani pakaza vizuri mchanganyiko wote kisha weka pembeni kwa masaa 3.
Katakata vitunguu maji, viazi, biringanyi, hoho na nyanya vipande vidogo dogo.
Kaanga kitunguu maji kwenye sufuria vikiwa brown weka binzari zote na viazi kaangia kwa dk 5, weka maji kama vinashika chini. Weka nyanya funika iive kidogo kisha weka biringanyi na hoho. Wacha mpaka mboga zote ziive.
Chota mchanganyiko huo kisha weka ndani ya kuku.mjaze kisha chukua vijiti vya meno mshone kisha chukua mafuta pakaza kwenye bati ya kuokea.juu muweke kuku kisha mwagia mafuta kidogo kwa juu na oka moto wa 175c kwa dakika 45.
Related posts
3 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/afya/futari-ya-chapati-kwa-mchuzi-wa-kuku/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/afya/futari-ya-chapati-kwa-mchuzi-wa-kuku/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/afya/futari-ya-chapati-kwa-mchuzi-wa-kuku/ […]