Vipimo
Nyamna Ya mbuzi ya mifupA -1 Kilo
*Ngano nzima – ¼ kikombe
Shayiri zilizopaazwa (quacker oats) za tayari – ¼ kikombe
Kitunguu saumua(thomu/galic) na tangawizi – 2 vijiko vya supu
Kitunguu – 1
Mdalasini vijiti -2
Bizari ya jiyra (cumin powder/bizair ya pilau)- 1 kijiko cha chai
Bizari ya majano (haldi/kurkum/tumeric powder) -1 kijiko cha chai
Pilipili manga – 1 kijiko cha chai
Kidonge cha supu – 1
Chumvi – kiasi
Siki au ndimu -2 vijiko vya supu
Mafuta -¼ kikombe
Maji kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Chemsha nyama kwa maji kiasi mengi, tia chumvi, mdalasini, thomu-tangawizi na pilipili manga. Funika nyama ichemke hadi iwive nyama.
- Toa nyama nusu kutoka katika supu au yote ukipenda, kisha itoe mafupa yake na utie nyama katika mashine ya kupaaza (chopper). Isage kidogo kiasi cha kuvurugika isisagike sana. Weka kando.
- Tia shayiri katika supu iache iwivie kidogo pamoja na supu baada ya kutoa nyamaKatika kisufuria kidogo,
- tia mafuta katakata kitunguu ukaange hadi kianze kugeka rangi,
- tia bizari ya haldi na jiyra na endelea kukaanga kidogoIrudishe nyama katika supu, kisha tia kitunguu ulichokaanga, tia kidonge cha supu, tia siki au ndimu iache kidogo tu ichemke ikiwa tayari.
vitumbua
Vipimo
Mchele – 2 mugs
Tui la nazi – 2 mugs
Yai – 1 kubwa
Sukari – ½ mug
Hiliki – ½ kijiko cha chai
Hamira – ½ kijiko cha chai
Unga wa ngano – 2 vijiko vya chakula
Samli ya kupikia (au mafuta) kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Osha na roweka mchele kiasi masaa kuanzia mawili au zaidi.
- Saga mchele na tui kwenye mashine ya kusagia (blender) mpaka uwe laini usiwe na chenga.
- Tia hiliki, hamira na unga wa ngano saga tena mpaka uchanganyike.
- Mimina kwenye bakuli na uache uumuke kiasi.
- Ukisha kuumuka changanya sukari na yai
- Tumia kama kijiko 1-2 cha chai cha samli kwa kukaangia kila kitumbua.
- Mimina mchanganyiko kiasi kwenye kikarai maalumu cha kuchomea vitumbua.
- Kitumbua kikiiva upande mmoja, geuza upande wa pili mpaka kiwe tayari.
- Panga kwenye sahani. unaweza kula vitumbua vikiwa moto au vikipowa.
Related posts
3 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Information here to that Topic: afroswagga.com/afya/jikoni-leo-shurba-kwa-vitumbua/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/afya/jikoni-leo-shurba-kwa-vitumbua/ […]
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/afya/jikoni-leo-shurba-kwa-vitumbua/ […]