Inawezekana umeshakutana na hili neno huko mitandaoni lakini hujajua maana yake ni nini “Selfcare”, Selfcare ni hatua za kuchukua muda kujiangalia/kujihudumia wewe mwenyewe, mara nyingi huwa tunajisahau tunaangalia afya za wengine kuliko sisi wenyewe au tunaweka muda wetu mwingi kwenye kazi/biashara/kutafuta pesa na mahitaji mengine na kujisahau kujitunza wenyewe.
Kuna aina nyingi za selfcare mfano ni:
- Social Self-Care.
- Mental Self-Care.
- Spiritual Self-Care.
- Emotional Self-Care
- Physical Selfcare
Sisi leo tunaangalia sana kwenye physical ambayo hii inahusiana zaidi na muonekano pamoja na mwili, unapoutunza mwili wako basi utafikiri na kujisikia vizuri pia. Kujitunza kimwili ni pamoja na jinsi unavyoupa mwili nishati, muda unaopata wa kulala, ni kiasi gani cha shughuli za kimwili unazofanya, na jinsi unavyoshughulikia mahitaji yako ya kimwili. Hapa kuna baadhi ya maswali unaweza kujiuliza ili kutathmini afya yako ya kimwili
- Je, ninapata usingizi wa kutosha?
- Je, mlo wangu unachochea mwili wangu vizuri?
- Je, ninasimamia afya yangu?
- Je, ninafanya mazoezi ya kutosha
Baada ya kujua hayo yote na kama unayafanya vyema basi vizuri na kama huyafanyi vyema basi jaribu kubadilika, mambo mengine ambayo unaweza kufanya ni pamoja na
Kula Chakula Chenye Afya (Healthy Food)
- Siku za kawaida inawezekana unakula chochote tu ili mradi upate kula lakini hii weekend ukiwa umepumzika jaribu kuangalia nini unakula na ikiwezekana plan chakula chako cha week nzima ili usije ukala chochote tu kisichokuwa healthy.

Jali Ngozi Yako
- Kama ilivyo kwenye kula ngozi pia huwa tunaziburuza tu tukiwa na haraka zetu za kwenda shughulini, weekend hii chukua muda wako kujali ngozi yako, fanya skincare, kama unaweza nenda spa.
Fanya Mazoezi
- Ni muhimu hasa kwenye kutengeneza mwili na ngozi lakini pia inasaidia kukufanya uondoe uchovu wa week nzima na kuondoa mafuta ambayo ulikula week nzima, pia inasaidia kuchangamsha akili na ukaanza week yako vyema kabisa.
Safisha Kabati Lako
- Safisha kabati lako inawezakana week nzima ulikua unatupa tupa tu nguo, hakikisha unalisafisha na kutoa vyote visivyo vaa, panga unavaa nini week ijayo, itakupunguzia stress za asubuhi lakini pia kuvaa vyema kunakufanya ujisikie vizuri.
Mkawe na week njema na tuambie je wewe huwa unatumia weekend yako kufanya nini katika selfcare?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…