Leo tushirikiane hii water therapy, sote tunakunywa maji lakini tunatofautiana namna tunavyotumia kinywaji hiki. Mara nyingine unaweza kuwa na tatizo aidha kusumbuliwa na kichwa, uchovu, kupoteza mng’ao wa ngozi au hata tumbo kutokaa vizuri kutokana na gesi n.k na mtu akakuambia tu kunywa maji mengi bwana au haunywi maji ya kutosha lkn kumbe sio tu kunywa maji mengi: ni unakunywa maji mengi kwa mpangilio upi?!
Jaribu kufuata mpangilio huu ;
Asubuhi
Kabla hujaweka mdomoni chochote kunywa maji si chini ya lita moja ndani ya dakika chache, ideal na Maximum ni lita moja na nusu tumbo lijae ‘ndi’ achana na kichefuchefu utajisikia vizuri si muda mrefu. Ukishakunywa ukamaliza tu haya maji utajisikia utumbo umeamka utapata haja kubwa. Baada ya hapo endelea na ratiba zako zingine kama ni kuoga,mazoezi n.k kunywa kifungua kinywa chako baada ya dakika 45 au saa 1.
Masaa kadhaa baada ya kifungua kinywa na kabla ya mlo wa mchana
Muda huu utakunywa maji nusu lita (500mls) hadi robo tatu lita(750mls).
Iwapo yale maji ya asubuhi ulikunywa saa 12 had saa1 hivi basi mpaka saa 5 utakuwa umekojoa hata mara tano mkojo usio na rangi yaani kama maji, baada ya hapo utaanza kuwa na rangi. ukiona unaanza kuwa na rangi basi ni wakati wa kunywa maji mengine.
Alasiri
Muda huu utakunywa maji nusu lita (500mls) hadi robo tatu lita(750mls).
Baada ya mlo wako wa mchana usinywe maji. Baada ya saa moja au mawili ukiendelea na zoezi la kukojoa maji uliyokunywa kabla ya mlo unaweza kunywa maji mengine. hii inaweza kuwa saa 9 hadi saa 11 jioni.
Usiku
Unaweza kunywa maji kiasi tu mradi usinywe wakati unakula.
Unafaidikaje kwa kupangilia hivi unywaji wa maji mengi wakati huo huo?
- Unaamsha mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula asubuhi hivyo chakula kilichosimama katika mfumo kinatolewa nje ili kisiendelee kuchacha na kuzalisha bacteria wabaya.
- Unapunguza tindikali (asidi) zinazoweza kuwa zimechochewa baada ya chakula kukaa muda mrefu tumboni.
- Unapunguza uzalishaji wa gesi tumboni, tumbo kujaa gesi au kujisikia umeshiba sana.
- Unachangamsha mwili wako.
Baada ya muda mrefu wa kutumia maji namna hii unafaidikaje?
- Kuwa na ngozi inayong’aa kwa kuwa na afya, pia kupungua/ kumaliza chunusi maana viwango vya maji na mafuta kwenye ngozi vinakuwa katika uwiano. Hydration is the key.
- Unajisikia u mwepesi maana mwili unakuwa haushikilii maji maana maji yanakuwa mengi katika mifumo yako.
- Kuweza kudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu.
- Kuweza kupungua uzito au kudhibiti uzito.
- kupunguza sumu mwilini hasa zinazotokana na madawa na vyakula
- Kupunguza uwezekano wa maambukizi ya mara kwa mara katika mfumo wa mkojo.
Kutokana na majukumu ya kila siku saa zingine inakuwa ngumu kunywa maji mengi hasa kutokana na usumbufu wa kwenda msalani mara kwa mara na foleni za barabarani n.k, unaweza kuamka ukajiandaa kwenda kwenye shughuli zako ukiwa na maji yako umebeba ukifika unakoenda kunywa maji yako kwanza ndo uendelee na kazi hii utaepuka usumbufu wa kukojoa wakati upo njiani kwenye foleni.
Pia unaweza kuchagua siku chache katika wiki ambazo utakuwa unakunywa maji kwa mtindo huu, mfano unaweza kufanya Jumatatu,Jumatano na Ijumaa au ukafanya jumanne na alhamisi au ukafanya weekend.
Ukiwa katika water therapy ili kupata faida epuka kabisa matumizi ya vinywaji vyenye sukari.
Kunywa maji ya joto la kawaida, usinywe ya baridi sana (yaliyotoka kwenye fridge).
Tufollow Instagram @afroswagga
Twitter @afroswaggatz
na facebook AfroSwagga
Related posts
4 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More Information here to that Topic: afroswagga.com/afya/tiba-ya-maji-kwa-afya-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/afya/tiba-ya-maji-kwa-afya-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Here you will find 76242 more Info to that Topic: afroswagga.com/afya/tiba-ya-maji-kwa-afya-yako/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/afya/tiba-ya-maji-kwa-afya-yako/ […]