Kuanza kula mlo kamili ni bora ni kazi sana, wengi wetu tunashindwa kutokana na miundo ya Familia zetu tumezoa tukiamka asubuhi ni viporo,vitumbua nk, mchana ugali na usiku wali. Hii inatufanya tuishi kwa ajili ya kula na si kula kwa ajili ya kuishi.
Kama ungependa kuanza kula kwa ajili ya kula hizi ni njia chache za kukusaidia.
Anza kwa kuhesabu matokeo
– nini unapata kutokana na mlo unakula sasa? unapata matokeo chanya au hasi? wengi tunaichukia miili yetu kwa kuwa minene, vitambi na kuchukia baadhi ya maeneo ya miili yetu. Lakini haya si matokeo makubwa sana kuna yale ambayo si ya kuchekea kama
- matatizo ya moyo
- hatari ya kupata kansa
- kunenepa kupita kiasi
- kuanza kujichukia na mengineyo mengi.
Kisha fikiria faida za kula mlo kamili na bora
- kupunguza nafasi ya kupata magonjwa
- kujiamini
- kuwa productive
- kuwa na nguvu na vingine vingi vizuri
Tafuta motisha
- jifunze faida za vyakula mbalimbali hii itakusaidia kujua kipi kinakufaa na kipi hapana
- follow accounts zinazo elimisha kuhusu vyakula bora
- anzisha urafiki na watu wenye lengo moja na wewe
- jifunze kupika vyakula bora kisasa ili uweze kufurahia mlo wako
Anza taratibu
Kosa kubwa ambalo watu wengi wanalifanya ni kutaka kuanza kwa ukubwa na hii si kwenye chakula tu bali hata katika maisha yetu ya kawaida, huwezi kumuachisha mlevi pombe kwa ghafla atateseka anza kwa kupunguza milo fulani taratibu kama punguza kula sukari na chai na anza kunywa chai na sukari, punguza kula viporo au vitumbua badala yake tafuta mikate ya brown etc. kama umezoea kula unhealthy food kwa week nzima jaribu kupunguza ziwe ziku sita au tano taratibu mpaka utakapo zoea kabisa.
Gawanya – namna rahisi ya kuacha tabia mbaya ni kuzireplace na zile nzuri, replace unhealthy food na zile healthy food
- Kunywa green tea badala ya coffee
- maji na fresh juice badala ya soda
- mchele wa kahawia badala ya mchele mweupe
- mafuta ya nazi au olive badala ya yale processed ya kupikia.
Jifunze mapishi marahisi yenye kutumia muda mchache –
jifunze mapishi rahisi ya mlo kamili hii itakusaidia kuepukana na kukununua vitu vya madukani au junky food, fanya hii iwe tabia yako. unaweza kutafuta siku mbili au tatu ukapika vyakula vingi na kuvihifadhi kwenye fridge ili pale usikiapo njaa unapasha na kula instead of ya kwenda kununua chips au burger
Remba sahani yako – vyakula hivi vinaweza visiwe na sura nzuri sana usoni mwako kwaio jambo jema ni kujaribu kukifanya kiwe kizuri kadri ya uwezo wako na utakavyo weza kula, ongeza taste unazo zipenda, weka vitu vya rangi rangi kama carrot, hoho za kijani, njano, nyekundu etc.
Rudia hizi tips mara kwa mara na utajikuta umezoa.
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/dondoo/jinsi-ya-kuanza-kula-mlo-kamili-na-bora/ […]