Wengi wetu huwa tuna dhani kuweka dawa na kufanyia steaming ndio kutakuza na kufanya nywele zetu kuwa na afya, hivyo utakuta mtu ana weka dawa kila baada ya mwezi na kufanyia steaming kila baada ya week mbili. Hii ndio husababisha nywele kunyonyoka na kutokua na afya.
Dawa si nzuri sana kwa nywele zako hivyo una shauriwa kuweka dawa mara mbili au tatu kwa mwaka. Hii ina maana uweke dawa kila baada ya miezi sita hadi minne. Lakini swali linakuja je katika kipindi hiko chote ambacho nywele zina oteana na kukua uta fanyaje hili zisikatike? hizi ndizo tips muhimu za nini ufanye
1) Deep Condition – fanyia deep condition mara kwa mara hii itasaidia kurainisha nywele zako na kuipa nywele afya, wakati una fanyia deep condition ni vizuri ukaosha nywele na maji ya baridi na pia usikae kwenye moto, paka condition yako funga mfuko wa plastic na taulo juu kaa nalo kwa nusu saa osha.
2)paka mafuta ya nywele kila siku – hii ni muhimu mno kwa nywele zako uli kuzipa nywele unyevu na kurainisha ili kuzuia ukatikaji wa nywele ni muhimu uwe una paka mafuta mara kwa mara, na mafuta mazuri kwa ajili ya nywele ni mafuta ya kumiminika na si mafuta ya mgando. Eg olive oil ya maji au mafuta ya nazi ya maji.
3) Kata ncha- Kukata ncha kunasaidia ukuaji wa nywele pia husaidia kujaza nywele.
4) Suka misuko ambayo haikati nywele – ipo mingi sana una weza ku google “protective hair styles” ukaipata lakini pia nywele za kurudi nyuma “twende kilioni” husaidia mno ndio maana utakuta wanafunzi wengi wana nywele ndefu zilizo na afya.
5)Punguza kukaa/kutumia vitu vya moto – kutumia pasi au dryer kukaushia au kunyooshea nywele mara kwa mara kuna athiri nywele, nywele hupoteza ubora wake kutokana na moto. Hii huathiri hata zile nywele zinazo ota. Kama una osha nywele mara kwa mara ni vyema ukaziacha zikauke zenyewe na upepo.
Related posts
4 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Here you will find 48888 additional Information to that Topic: afroswagga.com/dondoo/namna-5-za-kudumisha-nywele-zenye-dawa/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/dondoo/namna-5-za-kudumisha-nywele-zenye-dawa/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/dondoo/namna-5-za-kudumisha-nywele-zenye-dawa/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/dondoo/namna-5-za-kudumisha-nywele-zenye-dawa/ […]