Kama ambavyo sote tunajua tumeambiwa tuepuke misongamano, kuna wale ambao wameambiwa wafanyie kazi nyumbani, kuna wale ambao wanaenda kazini lakini wana practice social distance etc.
Hii inapelekea wengi wetu kuwa nyumbani na kuwa karibu na vyakula, lakini pia kufungwa kwa sehemu za mazoezi ( gym ). Kuna aina mbili za watu watakao toka kwenye isolation, ambao watatoka wamenenepa na wale ambao watatoka na body goals chagua moja.
Leo tunakuletea namna ambavyo unaweza kurekebisha afya yako wakati tupo katika Isolation
- Kufanya mazoezi hakuhitaji gym
Kuna application mbalimbali za mazoezi ambazo unaweza kutumia kufanya baadhi ya mazoezi madogo madogo nyumbani, tenga muda wako kati ya asubuhi au jioni na ufanye mazoezi husika mfano: Kutembea tembea katika uwanja wa nyumba yako, Kuruka kamba, Squats hazihitaji kwenda gym lakini pia ni nzuri katika ku-improve immune zako na kutoka jasho ambapo ni moja ya vitu tunashauriwa kufanya ili kuepuka maambukizi ya Covid19

- Epuka Kula Un-Healthy Food
Wakati huu wengi wetu tunatumia kujisosomola kwa kula vyakula ambavyo si vizuri na afya zetu, badala yake chagua vyakula ambavyo vinafaa lakini pika vizuri. Mfano: Badala ya kunywa soda, tengeneza juice yako nyumbani. Instead ya kula chips za kukaanga na kuku, pika mchemsho wako vizuri, Badala ya kula biscuits na chocolate anza kula matunda kama apples au machungwa,
- Kunywa Vimiminika
Hapa hatumaanishi unywe soda au processed juice, hapa tunamaniisha kunywa juice ambazo ni fresh au muhimu zaidi ni kunywa maji. Maji sio tu yanasaidia katika ngozi yako lakini pia huwa yanaondoa uchovu. Lakini pia unaweza kuongezea vitu kama limao, tango, tangawizi ili kuinua immune system zako.

- Lala Vyema
Ikiwa unafanyia kazi nyumbani huitaji kuamka asubuhi subuhi kujiandaaa au hata kama unaamka asubuhi basi hakikisha una tenga masaa machache mchana kujipumzisha, kupata usingizi mchache kuna madhara mentally, physically na hata katika Immune system zetu. Hii haitasaidia tu katika kuepukana na COVID 19 bali pia katika kupumzisha mwili, akili na kufanya ngozi zetu ziwe bora

Well Afromates Stay Safe, Safisha Mikono Yako Kwa Maji Tiririka, Vaa Barakoa Unapokuwa Katika Misongamano, Practise Social Distancing Na Kuwa Healthy.
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…