Wakati wengi wamemaliza kufunga Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na kupungua uzito wengi watakuwa wanajiuliza namna ambavyo wanaweza ku-maintain mwili wako ubaki hivyo hivyo bila ya kuongezeka huku wengine wakiwa wanateseka na namna wanaweza kupunguza miili yao bila ya kufanya mazoezi na kufanya diet kali.
Kuna njia rahisi kama unaweza kujizoesha kufanya basi unaweza kupunguza uzito lakini pia kuwa na afya kipindi chote, hizi tumetoa katika life style ya wa China, China inasifika kwa kuwa watu wake wana afya nzuri unaweza kukutana na mzee ana tembea ana fanya mazoezi yupo fit lakini hii inatokana na jinsi wanavyo chagua kula na kuishi.
- Maji Mengi
Washauri wengi wa mambo ya afya wanashauri kunywa maji lita zaidi ya mbili kwa siku kama ungependa kuwa na afya nzuri lakini pia husaidia kupunguza uzito, unapo kunywa maji mara kwa mara kunakufanya uhisi shibe na kukufanya kuto kutaka kula kula au kutafuna tafuna mara kwa mara.
- Green Tea
Wachina wamekuwa wakiwa wamezingatia kunywa chai ya kijani kwa miaka mingi. Wanaamini kwa uwezo wake wa kusafisha mwili kutokana na sumu yoyote kwakuwa inaaminika kuwa na antioxidant nyingi. Zaidi ya hayo, kunywa kikombe cha chai ya kijani baada au wakati wa mlo husaidia kuondokana na tamaa ya kunywa vinywaji vingine visivyo na afya kama soda au mvinyo
NAMNA 5 ZA KUPUNGUZA UZITO BILA KUTUMIA NGUVU
- Kula Chakula Cha Usiku Kabla Ya Saa Mbili Usiku
Watu wengi huwa tunalala kuanzia saa tatu mpaka saa nne, ukila chakula baada ya saa mbili usiku inamaanisha chakula hakipati muda mzuri wa kumemenyeka kabla hujalala, wachina wengi hula chakula chao cha usiku kuanzia saa kumi na mbili na nusu jioni mpaka saa mbili usiku hii hufanya chakula chao kimemenyeke vyema kabla ya wao kwenda kulala. Hii ni tip muhimu sana kama ungependa kupungua bila ya diet.
- Chagua Vyakula Vya Kuoka Na Supu Zaidi Kuliko Vya Kukaanga
Mafuta si mazuri mwilini, kwetu wa Tanzania bila ya kula chakula cha mafuta iwe kukaanga au rost hatuoni kama tumekula hii inasababisha mafuta kugandiana mwilini na kuongezeka mwili, kwa wenzetu wao wanachagua au upendelea kula suop na vyakula vya kuoka zaidi ambavyo huwa vina mafuta kidogo mno na viungo vichache katika kupikia.
Tips Za Kupungua Uzito Ndani Ya Siku 7 – Khloe Kardashian
- Kutumia Vyombo Vidogo
Kama huwa unaangalia movie au kufuatilia vipindi vya kichina utakuwa umegundua wachina wana kawaida ya kutumia vyombo vidogo, iwe sahani, bakuli au kikombe hii ni kutaka kuto kupakua vyakula vingi kuna msemo usemao “smaller bowls = smaller portion” lakini pia kama unavyombo vikubwa basi jitahidi kujikadiria chakula cha wastani na sio kutaka kujaza chakula kutokana na ukubwa wa chombo chako.
- Matunda na mboga mboga
Kula mboga mboga na matunda kunasaidia pia kufanya mwili wako upungue na uwe na afya nzuri, unaweza kula mboga mboga kama main dish na kula matunda pale unapo jisikia hamu ya kula kitu kingine baada ya kula main dish hii husaidia kutokula vitu visivyo na afya kama chocolates na biscuits.
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you will find 20909 additional Info to that Topic: afroswagga.com/dondoo/njia-6-rahisi-za-kupunguza-uzito-bila-ya-kutumia-diet/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/dondoo/njia-6-rahisi-za-kupunguza-uzito-bila-ya-kutumia-diet/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/dondoo/njia-6-rahisi-za-kupunguza-uzito-bila-ya-kutumia-diet/ […]