Maharagwe imekuwa ni nafaka inayoliwa na watanzania tulio wengi hasa kutokana na kipato chetu. Lakini leo nataka nikwambia faida ipatiakanayo kwa matumizi ya nafaka hii katika afya mwanadamu. Hakika si wengi tuliokuwa tunaijua siri hii, ndio maana nimeona haja ya kushirikiana na nyinyi katika Makala hii ndogo inayohusu maharagwe. Najua tulio wengi tunayajua maharagwe na makundi yake kadhaa.
Tafiti mbalimbali zimefanywa na wataalam wa maswala ya sayansi ya lishe na kupata majibu kadhaa ambayo leo nataka na wewe msomaji wangu upate kuyafahamu ili kama hupendelei kula maharagwe basi uanze mara moja pindi tu utakapomaliza kusoma Makala hii. Zifuatazo ni faida zipatikanazo kwa kula maharagwe;
1. Kudhibiti uzito wa mwili
Katika uchunguzi wa hivi karibuni wa jarida la American Collage of Nutrition umebaini kuwa watu wanaokula maharagwe wana 22% ya kupunguza uzito wa mwili. Na wana uwezekano mkubwa wa kuwa na viuno vidogo kuliko watu wasiokula kabisa maharagwe. Maharagwe yana kiasi kikubwa cha nyuzi nyuzi zinazozoyeyuka, ambazo zinapunguza kasi ya mmeng’enyo wa chakula na kukufanya kutosikia njaa kwa muda mrefu.
2. Yanaongeza madini ya chuma
Maharagwe ni chanzo kizuri cha vitamin C ambayo yanaongeza uwezo wa mwili katika kufyonza chuma.
3. Kupunguza hatari ya kupata saratani
Katika kuangalia takwimu za lishe ya wanawake 90,630 wenye umri kati ya 26 hadi 46 katika chuo kikuu cha Havard Kitivo cha Afya ya Jamii, matokeo yalionyesha wanawake waliokuwa wakila mharagwe angalau mara mbili kwa wiki, wana asilimia 25 ya kupunguza hatari ya kupata saratani ya matiti, kulingana na wanawake wanaokula mharagwe kwa mwezi.
4. Kuthibiti mapigo ya juu ya moyo
Katika utafiti mwingine uliofanywa na wataalum wa nchini Australia, ulibaini kuwa protini iliyopo katika maharagwe na nyuzinyuzi zinazoyeyuka hudhibiti mapigo ya moyo kuwa juu.
5. Yanapunguza hatari ya Ugumba
Ulaji wa maharage upunguza athari za wanawake kupata ugumba.
Mwisho nivema kujizoeza kula walau jamii moja wapo ya maharagwe kwani zipo nyingi mno, manufaa yake ni mengi mno katika miili yetu. Asante
Imeandaliwa na
Salma Machozi
M: +255 713 002553
E: machozisalma519@gmail.com
Related posts
6 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you will find 31783 more Info to that Topic: afroswagga.com/dondoo/umuhimu-wa-maharagwe/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Information here to that Topic: afroswagga.com/dondoo/umuhimu-wa-maharagwe/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here to that Topic: afroswagga.com/dondoo/umuhimu-wa-maharagwe/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/dondoo/umuhimu-wa-maharagwe/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Information here on that Topic: afroswagga.com/dondoo/umuhimu-wa-maharagwe/ […]
… [Trackback]
[…] Find More here on that Topic: afroswagga.com/dondoo/umuhimu-wa-maharagwe/ […]