Tulifanya interview na Nuru the light kuhusu kurudi kwake katika mitindo, style zake za fashion lakini pia alituambia wimbo wake mpya ameshatoa video na tukamsupport kwa kuungalia youtube oh well oh well kama Afroswagga tukasema twende tukaiangalie lakini pia tuifanyie review ya fashion zilizomo mule ndani.
Tulicho gundua mitindo uliyo tumika ni kawaida mtu yoyote anaweza kuvaa (easy to copy) lakini pia trend nyingi zimetumika kama Flare na Fur. Katika Video hii Nuru amekuwa styled na Stylist Irfan Rizwanali ambae tumepata fursa ya kuongea nae mawili matatu
Afroswagga – what’s was the story behind the outfit?
Irfan – Tulipokuwa tukifikiria mavazi, mimi nilikuwa nawaza tu jinsi ya kumfanya awe tofauti na jinsi alivyokuwa akionekana katika video zake zilizopita. Jinsi ya kuwiana mavazi ya sasa hivi pamoja na aina ya mwili wake ili kufunika kasoro zake, pia niliwekea maanani rangi yake ya ngozi, uso wake na muhimu zaidi mandhari ya wimbo
Afroswagga -tumeona umetumia trends like flare, fur kwanini umechagua hizo?
Irfan- Kwasababu mwaka 2018 ni mwaka wa kuvunja mipaka ya frikra katika mitindo, nilijua nilitaka awe katika mavazi ya kisasa na ya kuvutia. Manyoya ni kipengele kimoja ambacho hakiwezi kamwe kupitwa na wakati. Tulitumia koti la kiofisi na kuwiana nalo na sketi ya manyoya ambayo haijawahi kuvaliwa na msanii yeyote, Pia tumetumia rangi zilizotulia ambazo ni rangi za msimu wa sasa ili zilingane na skintone yake (rangi yake ya ngozi).
Tumetumia magauni yaliyochanua ili kumfanya aonekane na rangi na mwili mzuri na mrefu zaidi. Nguo zilikuwa na rangi ambazo zimetulia sana tukizingatia taa zilizotumika na wapiga picha na eneo ambalo video imefanyika
Afroswagga: ilikuaje kufanya kazi na Nuru?
Irfan: To be honest I never knew who Nuru was, till when I got a call from the producer a day before the shoot saying they wanted to hire me to be her Stylist.
She is one amazing lady, we connected staright away when we meet. She smart , educated and very down to earth. And the most amazing thing is she is ever ready to push the envelope. We had an amazing time working together
Afroswagga- Unawashauri nini wasanii wakiwa wanafanya video zao? wazingatie kitu gani katika mavazi?
Irfan- Wanamuziki karibia wote niliowaona au nawajua, kwa kawaida hufuata mwenendo wa kimitindo wa watu maarufu wa Hollywood. Kuhamasishwa ni kitu tofauti, lakini kuhamasishwa kwa kiwango ambacho unaanza kuiga jinsi wanavyovaa ni a Big No No. Hapana kwa kweli.
Wakati wa kupanga nguo za kuvaa kwa ajili ya wimbo, wanapaswa kukumbuka kila kipengele cha wimbo kwa undani zaidi, wimbo unahusu nini? Wimbo unahadithia nini? Je! Dhana ni nini na muhimu zaidi ni maeneo gani wanaenda kufanya video ya wimbo?
Mbali na hilo, pia msaani anatakiwa azingatie aina ya mwili wake, rangi ya ngozi na ana kasoro gani. Mambo haya yote ni muhimu sana.
Kuwa wa asili, original, tengeneza mwenendo wako mwenyewe na muhimu zaidi tumia rangi na mavazi ambayo yanaendana na wewe.
unaweza kuangalia video hapa
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/fashion-cop/amfvr-umeniacha-by-nuru-the-light/ […]