Ikiwa tunaona tasnia ya mitindo inaanza kurudi katika heshima yake kutokana na maamuzi mbalimbali yaliyo chukuliwa hivi katibuni kama kuwa na chana cha mitindo, bi. Asya Khamsin na Hashim Lundenga kuwaachia vijana kusimamia majukwaa yao ya mitindo kuna wengine ambao bado wamekwama katika Dunia ya zamani, mitindo ya zamani.
Sio mbaya sababu kila mtu ana style yake katika swala zima la fashion lakini saa nyingine ina bidi kuangalia muda, nini kipo wakati huo na nini unataka kufanya,well seems like wasanii wa zamani wanajaribu kutoka kurudi tumeona picha kutoka kwa nuruelly akiwa na Banana Zorro na Kala Jeremiah ni kama wapo location kwa ajili ya video ya wimbo wao mpya, tuna furahi kuona wasanii wa zamani wakijumuika pamoja na kutaka kurudisha ile ladha ambayo wengine tunaimiss. Lakini pia tungefurahi zaidi kama wange jaribu ku-keep na Dunia ya sasa katika mitindo.
Hawa wasanii wa sasa wanajitahidi sana katika kuvaa japo kuna sehemu wanakosea lakini tulipo sipo kule tulipo toka, na hatutaki kurudi kule kuna wengine ambao huwa wanaangali music video kwa ajili tu watu wamependeza, na wengine wanampenda msanii na huku wengine wakipenda wimbo well kama msanii inabidi uwaridhishe mashabiki zako wa aina zote, Nuruelly, Banana Zorro na Kala Jeremiah wame tu-disappoint kwa kiasi kikubwa na tuna hope kwamba hii video ikitoka basi wawewamefanya haya marekebisho.
The suits ni za zamani mno, nani anavaa these kinds of suits with this kind of fabric these days? tulisha papita hapa zamani sana. Hizi fabric zilikuwa zinavaliwa zamani hasa kama mtu anaoa, hakuna mpangilio mzuri katika mavazi kama utaangalia kuna ambae ana tai, mwingine vifungo kafunga nusu, wengine wana mikanda wengine hawana, tunadhani bado hawajapata taarifa ya kwamba kuna stylist siku hizi, lakini swali letu kubwa ni kwamba kwanini suit ya aina moja? hata kama ni band music waangalieni basi hata saui sol jamani siku hizi tunachanganya vitu kila mtu na mavazi yake to make it more interesting.
Kwetu sisi hizi ni outfit mbaya toka mwaka uanze hasa katika upande wa wasanii wa kiume Tanzania, tukiwa tunapigia kelele wasanii wa kike kwenda gym tuna sahau wa kiume pia, Banana na Nuruelly inabidi gym iwahusu au mjaribu ku-keep up na dunia ya mitindo, Rick Ross amepungua, Dj Khaled ana jaribu kwenda gym kwanini sisi tushindwa?
Kurudi kwa wasanii kuna hitaji a big punch katika kila sekta yaani macho yote yawe kwenu lakini kama hapa tu tumeona kasoro mnadhani tutakuwa interested na kujua kinacho taka kuja? Igeni mfano wa Nguza Viking na Papii hawaja kurupuka na wao ndio walikuwa ndani kwa miaka zaidi ya kumi na wamerudi wameelewa dunia ina taka nini.
Nguza na Papii wamatafuta mbunifu ambae ameweza kuwapa mionekano ya kisasa ambayo inaendana na muziki wao.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…