Mpaka sasa wasafi festival imeshapita sehemu tatu ambapo walianza na Mtwara, wakaenda Ruangwa na week hii tumewaona wakiwa Songea, na tupo hapa kuongelea looks za recently ambayo ni Songea, utajiuliza kwanini tumeruka Ruangwa, sababu ni moja tu hakukuwa na looks za kuziongelea sana.
Songea wasanii walijiandaa, we love ambacho tumekiona, stage zilikuwa za moto makes us wonder wakimaliza Dar itakuwaje, let’s get back to the looks.
Creative looks kutoka kwa Diamond Platnumz ambae yeye alivaa kama mfungwa, G nako alikuwa na mavazi ya ki-asili huku Mbosso yeye akiwa amevalia all white looks ya taulo na vest’s wali stand out na kuwa tofauti na wengine.

Patches & Graphic Looks kutoka kwa Chegge, Lava Lava & Mh Temba, tumependa hizi looks maana zipo ki-stage zaidi, zimefanya wa stand out na waonekane kama watumbuizaji siku hio

Classy looks kutoka kwa Ommy Dimpoz, Ray Vanny & Whozu, hizi ni neat looks hawa alivaa suit na suruali za vitambaa, ikiwa Ommy na Whozu wakichagua nguo nyeusi, Rayvanny yeye alikuwa na full red

Colorful Looks kutoka kwa Darassa, Billnas na Baba Levo, yes kupanda jukwaani unaweza kujikuta umevaa sare na shabiki inabidi u-stand out moja ya kitu kinachoweza kukutofautisha na mashabiki ni chaguzi za rangi na hapa tunaona namna Darassa na Baba Levo walivyochagua nyekundu wakati Billnass yeye alikuwa na orange na white look.

Kama kuna muonekano haupo hapa ni kwamba tumesahau au haukutu-impress lakini pia tunajua tumemuacha Zuchu huyu ana article yake binafsi, tuambie muonekano upi umeupenda zaidi?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…