Miili imekuwa kisingizio cha wengi kutokuvaa na kupendeza, lakini kumbe kila mmoja wetu anaweza kuvaa na akapendeza inatakiwa tu uujulie mwili wako wa aina gani na mavazi yapi yanakufaa, kama ungependa kujua zaidi kuhusu aina ya mwili wako na mavazi yapi yana kufaa tunashare link hapo chini ukasome.
Lakini hizi ni Dondoo 5 ambazo tumekuandalia kiujumla kama una mwili mnene zinaweza kukufaa
- Crop It
Vaa crop top yako na high waist pants au skirt kutengeneza shape, high waist trouser zinakusaidia kukupa muonekano wa kiuno chembamba.
- Flare it
Flared pant will never go out of style, ni vyema ukawa nayo katika kabati lako. Hakikisha unaivaa na top fupi au chomekea kukupa balance ya mwili wako na outfit yako, kama si mpenzi wa suruali, kuna flare dresses pia.
- Wrap it up
Wekeza katika wrap dresses au wrap tops, Wrap dress ni kama flare pants ni vyema ukawa nazo katika kabati lako, husaidia kutenganisha kifua na kiuno na kukutengenezea muonekano mzuri wa mwili wako.
- Chagua Material Sahihi Ya Mavazi Yako
Kama wewe ni mpenzi wa mavazi yenye material membamba inabidi uachane nayo na kuanza kununua mavazi ambayo yana material nene kidogo kama, spandex na neoprene material. Sababu material haya yanakufanya uonekane slim kuliko ambavyo upo.
- Usifiche Mwili Wako
Wengi wenye miili hii huwa tunachagua mavazi makubwa kuliko sisi, tukidhani zinatupa muonekano mzuri lakini kumbe zinazidi kutuficha na kufanya miili yetu izidi kuonekana mikubwa, badala yake chagua mavazi ambayo yana kufit vyema na kuonyesha sehemu ambazo unadhani zina favor mwili wako. Yaani kama una miguu mizuri basi vaa nguo inayokufit vyema lakini fupi ionyeshayo miguu, kama ni mabega basi fanya hivyo pia n.k
Picha zote zilizotumika ni za @ms.chicca_bwase
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/habari/dondoo-5-za-mitindo-kwa-watu-wanene/ […]