‘Kweli iliyo uchungu si uwongo ulio mtamu’ Diamond Platnumz.
Kadri miaka inavyokwenda tumeendelea kuona kusifiana uwongo, na uwongo umeonekana kuwa mtamu zaidi ila uchungu umegeuka katika upande wa ukweli na wengi kuona ukweli ni mbaya katika maisha yao.
Hii inafanya kuona wasanii wengi wapo sahihi katika mambo mengi, ila katika uhalisia ni wazi wamekuwa wakipotoka katika mambo mengi. Afroswagga tumejikita zaidi katika upande wa mavazi (Fashion) na daima tunasimama katika ukweli sisi sio watu wa uwongo mtamu kama walivyo wengine.
Kila mmoja amekuwa akiongea juu ya wimbo wa Salome ambao ni wimbo mpya wa Diamond Platnumz, kiuhalisia ni wimbo mzuri.
Ila katika upande wa video ni wazi umekuwa si upande mzuri kama ambavyo wengi wao wenye uwongo ulio mtamu wanavyoendelea kuhubiri tangu kutoka kwa wimbo huo.
Sisi tunafananisha video hiyo na msemo usemao “Shoka lisilo na mpini halichanji kuni” Tukiwa na maana muziki ni njia moja wapo ya kutangaza vitu vingi katika nchi husika, vitu hivyo vyaweza kuwa mavazi, utamaduni, vyakula, na mengine mengi.
Katika upande wa Diamond kwenye video ya Salome tumeona akiwa amevaa mavazi ya Nigeria. Hatuwezi kusifu juu ya muonekano wake katika video hiyo maana nguvu aliyotumia kutangaza mavazi ya Nigeria ni wa hali ya juu.
Ikumbukwe leo hii ukiona tu mavazi ya Nigeria, Uganda, Ghana hizo ni baadhi ya nchi ambazo wasanii na watu wao maarufu wamekuwa wakitumia sanaa zao katika kutangaza mavazi yao.
Tunafahamu kama nchi yetu hatuna vazi la taifa ila yapo mavazi ambayo ukivaa unaonekana wewe ni mtanzania, hivyo ni vyema Diamond Platnumz kuamka kifikra wimbo kama Salome ilipaswa kuutendea haki kwenye video kama ambavyo aliutendea haki mmiliki halali Saida Karoli
imeandikwa na @batro15
tupe Maoni Yako kupitia
Instagram – AFroswagga
Twitter – Afroswaggatz
Facebook – Afroswaggamag
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…