Zulfa Yazid Suleiman (20) hivi karibuni alishinda kuwa Miss Kyelwa 2021, Zulfa amezua gumzo katika mitandao ya kijamii kutokana na uchaguzi wake wa mavazi aliyoyavaa katika uzinduzi wa Jengo La Mkuu Wa Wilaya ya Kyerwa.
Katika uzinduzi huo, Zulfa alichagua kuvaaa ripped jeans, stripped tshirt na raba, kitu ambacho kilizua gumzo kutokana na kwamba mavazi haya hayaendani na tukio alilokwenda kuhudhuria. Tulitegemea kumuona akiwa smart kimavazi kutokana na taji lake alilotunukiwa lakini pia ukiangalia wengine wote waliohudhuria tukio hili walikua wamevalia kuendana na tukio huku wengi wao wakiwa na umri mkubwa kuliko yeye.

Hii imesababisha tujiulize Je kosa ni la Zulfa au waandaaji na management yake? Kwanini aliruhusiwa kutoka akiwa amevaa mavazi haya kwenda kwenye tukio kubwa kama hili? Je Zulfa mwenyewe kwakupenda kwake urembo mpaka kwenda kushiriki Miss Kyerwa na kushinda taji hilo, hajui ni mavazi ya aina gani yavaliwe wapi mpaka akamua kuvaa mavazi haya?

Ukiangalia vizuri utagundua Zulfa amevaa sash zake zote mbili tena kwa mtindo wa X, Je hakufundishwa namna nzuri ya kuvaa hizi sash? Well tunadhani kupitia kwa Zulfa wengine pia watajifunza lakini pia management ya hawa warembo tungependa muwe mnawapa warembo wetu taarifa mapema na namna wanatakiwa wajiweke ikiwa wanabeba sura ya sehemu husika.
#Afromates tuambie hapo chini unadhani nani wa kulaumiwa?
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/habari/gumzo-juu-ya-mavazi-ya-miss-kyerwa-2021/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Info here on that Topic: afroswagga.com/habari/gumzo-juu-ya-mavazi-ya-miss-kyerwa-2021/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Info here to that Topic: afroswagga.com/habari/gumzo-juu-ya-mavazi-ya-miss-kyerwa-2021/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 1974 additional Info to that Topic: afroswagga.com/habari/gumzo-juu-ya-mavazi-ya-miss-kyerwa-2021/ […]