Ikiwa ni siku chache tu toka atwae taji la Miss Tanzania Mwanadada Diana ameanza kulalamikia uongozi wa Miss Tanzania kwamba kuna mengi yana hitaji kufanyika na hapewi support ya uhakika, hili lime kua tatizo kwa miaka nenda rudi nadhani ni wakati wa waandaji wa shindano hili kubadilika.
Diana alikuwa na haya ya kusema wakati akihojiwa katika kipindi cha planet bongo east africa radio
“Hata zawadi zangu zilizo haidiwa sijapewa, kwahiyo inakuwa ngumu kwangu kujiandaa na mashindano ya miss dunia,” Diana alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio. “Siku ishirini zilizobaki ni ndogo natakiwa kuandaa documentary ya historia ya kimasai Arusha. Sina kitu chochote chakufanyia natakiwa nilipe hiyo, natakiwa nilipe team support kwa sababu natakiwa kwenda kuonyesha Tanzania yangu, natakiwa kuonyesha beauty of purpose,”
Aliongeza, “Tanzania, viongozi, serikai, Miss Tanzania cometee, i need suport, i need what i deserve, unajua mimi ni mtu ambaye najiongeza, kwa hiyo nikipewa suport kidogo i push it up, kuna watu ambao nimewaomba suport wamenipa vya kutosha, kwa hiyo i need what i deserve”
Kwa upande wa afisa uhusiano wa kamati ya Miss Tanzania, Hidan Rico amesema shughuli za maandalizi ya miss huyo zinafanywa na Kamati ya Miss Tanzania.
“Hayo mambo yanashughulikuwa na Kamati ya Miss Tanzania. Yaani ameshaanza kuongea na vyombo vya habari? Mimi sina mamlaka ya kulijibu hilo la zawadi lakini nachojua maandalizi yake yanafanyika na kamati,” alisema Rico.
tupe moani yako kupitia
Instagram – afroswagga
Facebook – afroswaggamag
Twitter – afroswaggatz
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…