Huko Uturuki habarikubwa ni hii ya Mahakama kwenye mji wa Istanbul kumhukumu mshindi wa zamani wa shindano la urembo nchini Uturuki kwa kosa la kumtukana rais wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdogan.
Kwa mujibu wa BBC Swahili , Merve Buyuksarac mwenye umri wa miaka 27 alipatikana na hatia ya kumtukana hadharani President wa Uturuki hivyo amehukumiwa kifungo kilichoahirishwa cha miezi 14 gerezani.
Inasemekana pia mrembo huyu aliandika kwenye mtandao wake wa kijamii pamoja na kuwatumia watu shairi lenye matusi katika mtandao wake wa Instagram lakini Wakili wake amesema wamepinga hukumu hiyo katika Mahakama kuu ya bara la Ulaya na Buyuksarac amekanusha madai yote dhidi yake.
Wanaharakati wa kupigania haki za Binadamu wanasema hiyo kesi ni njia ya serikali ya rais Erdogan kukandamiza uhuru wa kujieleza ambapo hadi sasa watu 2000 wengi wao wakiwa ni Wasanii nyota na hata wanafunzi wameshtakiwa kwa kumkejeli au hata kumtusi Rais huyu tangu mwaka wa 2014.
BBC wameripoti kwamba hukumu hiyo iliahirishwa ilimradi tu asirudie makosa hayo katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Related posts
2 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/habari/miss-uturuki-hatiani-kwa-kumtukana-rais/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/habari/miss-uturuki-hatiani-kwa-kumtukana-rais/ […]