Kwanza kabisa tuanze na hongera kwa Yanga kwa kututoa kimasomaso baada ya miaka mingi kupita, kama Nchi tuko proud na hii achievement.
Turudi kwenye vazi la Yanga huko white house walipopata mlo wa usiku na Rais, Samia Suluhu. Yanga walifika wakiwa wamevalia nguo zao za mazoezi za Yanga walivaa jersey na sweat pants zenye logo zao. Kwa jicho letu la fashion tuliona haikukaa sawa tukauliza kwenye social media zetu na tulipata majibu tofauti tofauti, wengine wakisema hapana wangejitahidi kuvaa mavazi mazuri huku wengine wakisema walikua wanasafiri usiku huohuo kwahio walichovaa hakikua na shida.
Kwetu tunaona wangejitahidi kuvaa mavazi mazuri, hata white shirt’s na suruali nyeusi wakavaaa na moka zao nyeusi wangependeza, utajua kwamba wao ni Yanga hawaitaji kuvaa jersey kujulikana kama wao ni Yanga.
Kuhusu kusafiri wangeweza kuwa na haya mavazi kwenye bus lao wakabadilisha wakishamaliza na dinner, ili kuwa comfortable na safari tunadhani hakuna kati yao ambae angeshindwa kubadilisha mavazi mbele ya mwenzie as we all know wachezaji wa mpira wanavaaga na kubadilisha mavazi changing room pamoja.

Unaenda kukutana na Rais wa Nchi Ikulu na umevaa sweat pants? ni jambo kubwa ambalo lilikuwa linatakiwa kuwekewa uzito kidogo, kwa wanaosema walishtukizwa tunadhani hakuna mchezaji hata mmoja ambae anaweza kukosa shirt nyeupe na official trouser na viatu vizuri vya kwendea kwenye jambo zito kama hili.
Picha ya kumbukumbu ambayo imepigwa inaonekana kuwa na mambo mengi, kwa maana kila mtu kavaa chake, kuanzia viatu mpaka mavazi huyu kavaa viatu vyeupe, mwingine kavaa vyeusi, huyu ana sweat pant ina prints huyu ana nyeusi tupu, wakati wangevaa vitu vya kueleweka basi picha nayo ingekuwa na uzito kidogo.
Anyways hayo ni maoni yetu tupe ya kwako hapo chini je umeonaje kuhusu mavazi yao haya?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…