Wengi wetu tunapenda urembo, lakini kwa bahati nzuri au mbaya wa afrika tume barikiwa na nywele ngumu hii ime tupelekea kupenda kuweka dawa za nywele ili kuzilainisha na kuzipa muoneka mzuri, lakini dawa hizi zina uzuri na ubaya wake.
Sayansi inaonyesha kuwa matumizi ya relaxer za nywele yanaweza kusababisha au kuongeza hatari ya kupata magonjwa ya moyo, kupungua kwa uwezo wa kiakili katika kufikiri na kupambanua mambo, kuungua kwa ngozi ya kichwa na muwasho wa ngozi. Matatizo mengine ni saratani ya matiti, mabonge katika mji wa mimba (Leiomyomata), upungufu wa kinga ya mwili na kubalehe mapema kwa wasichana. Katika utafiti uliofanywa na wanasayansi Lauren A. Wise na wenzake (Wise et al, 2012: Hair Relaxer Use and Risk of Uterine Leiomyomata in African-American Women) na kuchapishwa katika jarida la American Journal of Epidemiology (2012) vol. 175(5):432-440, ilibainika kuwa matumizi ya relaxer yanaongeza hatari ya kupata mabonge katika mfuko wa kizazi.
Mabonge yanaweza kusababisha ugumba hasa pale yanapokuwa makubwa na kulazimisha tiba ya upasuaji ya kuondoa kizazi (hysterectomy). Katika jamii za wanawake wanaotumia relaxer kwa kiwango kikubwa, chanzo kikubwa cha upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi ni mabonge. Inasemekana kuwa katika nchi ya Marekani wanawake weusi wanakabiliwa na tatizo la mabonge mara mbili hadi mara tatu zaidi ya wanawake wengine. Hii inaweza kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na matumizi makubwa ya vipodozi kama relaxer.
Viambato vilivyomo ndani ya dawa hii hupenya na kuingia katika mfumo wa damu na kwenda kuvuruga mfumo wa vichocheo vya ujinsia hasa homoni za kike. Relaxer nyingi za nywele zina kiwango kikubwa cha kemikali kama vile lye (Sodium hydroxide au Caustic soda), calcium hydroxide, guanidine carbonate, thioglycolic acid salts na monobutyl phthalate.
Related posts
4 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Here you will find 42043 additional Information to that Topic: afroswagga.com/hair/madhara-ya-dawa-za-nywele/ […]
… [Trackback]
[…] Here you will find 62759 more Info on that Topic: afroswagga.com/hair/madhara-ya-dawa-za-nywele/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/hair/madhara-ya-dawa-za-nywele/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 64572 additional Info on that Topic: afroswagga.com/hair/madhara-ya-dawa-za-nywele/ […]