Kuna wale wenzangu na mimi tukitoka tunawaka, nywele kali, ka-makeup usoni, tunanukia mpaka tunavutia majini lakini ukifika nyumbani tu hali inabadilika, wig imetupwa kushoto una mabutu yako yana miezi mitatu, unatoa nguo unachukua ki-khanga chako kimepaukaa, unukie au uoge unaenda wapi kwani? upendeze unam-pendezea nani? ukisikia hodi unanuna huyu nae nani mi niko hovyo lol, kama unavyoendelea kusoma ndio unajiona kabisa ni wewe na ungependa kuacha hii tabia basi hizi tips 3 zitakusaidia,
- Fresh Up A Liltle Bit
Huitaji makeup ukiwa nyumbani lakini haimaanishi usiwe vyema, kuoga sio mpaka utoke oga vizuri,paka perfume, perfume sio tu kwa unaokutana nao bali hata kwako pia ukinukia vyema unajisikia vyema, chana nywele au suka minyoosho yako mizuri, fanya skin care, huwezi kupaka lipstick basi hata ka lip balm ka hapa na pale hakadhuru,
- Upgrade Mavazi Yako Ya Kushindia Nyumbani
Mavazi ya ya kushindia sio ndio yawe yale yaliopauka ambayo unaona huwezi kutoka nayo nje, mgeni anakuja una khanga imechanika au t-shirt ya msiba toka mwaka juzi imefubaa, nunua mavazi mazuri ya kushindia nyumbani mfano lounge wear, two piece sets, leggins & tank top, tank dress, casual 2 pieces set etc

- Upgrade Mavazi Yako Ya Kulalia
Hapa ni sawa tu na mavazi ya kushindia sio kwasababu unalala usiku basi ndio uvae mavazi hayaeleweki hata ukitokea moto usiku ushindwe kutoka nje, hakikisha mavazi yako ya kulalia mazuri na ni comfortable mfano satin payjamas, silk satin sleep wear inaweza kuwa gowns au set inategemea na mapenzi yako

Huitaji kununua haya mavazi kwa gharama kubwa unaweza kununua hata mtumba lakini yawe na quality nzuri.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…