Wengi tunashindwa kujua tuanzie wapi na tuishie wapi katika kununua mavazi,na hii inapelekea kuwa na nguo nyingi ambazo haziwezi kujirudia unavaa mara moja hujui uvae wapi tena, well leo tunakuletea vitu 5 muhimu kuwa navyo katika kabati lako ambavyo ni kama msingi wa kuelekea kuwa stylish & classic wear.
- Plain White Tee / Shirt
T shirt au shati nyeupe ni muhimu kuwa navyo katika kabati lako, ni kutokana na kwamba inaweza kuvaliwa na chochote iwe suruali ya kitambaa, jeans, skirt, culottes, pensi nk, lakini pia inaweza kuwa casual na smart wear. Kabati lako si kamilifu kama bila ya kuwa shirt au t-shirt nyeupe.
- Perfect Jeans
Iwe skin jeans, mom jeans, iwe flared au cropped ili mradi ni jeans ambayo ina ku-fit vizuri basi ni muhimu kuwa nayo, kizuri kuhusu jeans nazo ni moja essentials ambazo zinaweza kutumiwa zaidi ya mara moja kama ni mzuri wa ku-style unaweza kuvaa hata week nzima,casual na hata business wear. Kingine unaweza kuvalia flats au heels inategemea na chaguo lako.
- Blazer
Hata kama hufanyi kazi katika ofisi , kila mwanamke anapaswa kuwa na angalau blazer moja ambayo ina mtosha vizuri, kama haikutoshi sawia hapo ndipo itabidi utafute fundi wa kukurekebishia, blazer inakufanya uonekane well polished na mostly smart.
Kwa upande wa viatu una paswa kuwa na
- Viatu vurefu (Heels )
kila mwanamke anapaswa kuwa na angalau pear mbili za viatu virefu Viwe ni pumps au strappy sandals. Viatu virefu vinakufanya uonekane jasiri, lakini pia vianakuongezea kimo. unaweza kuwa na pear hizo mbili za rangi nyeusi na nude. lakini kwa wanawake huwa hatuna enough shoes unaweza kuwa nazo nyingi uwezavyo.
- Ballet Flats
Kuna sababu kila mtu anapenda kuvaa ballet flats, vinakufanya uonekane chic & smart . Unaweza kumiliki viatu hivi kwa rangi mbalimbali pia unaweza kuvaa na jeans na mavazi tofauti tofauti, kikubwa ni kwamba ballet zipo comfortable & rahisi kutembelea.
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Information here to that Topic: afroswagga.com/mitindo/5-wardrobe-essentials-you-should-own/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/5-wardrobe-essentials-you-should-own/ […]