Well dressed woman anaonekana yaani ukimuona tu unajua huyu dada anajua kuvaa, na hii inatokana na wao kujua nini wanunue,nini wasinunue, nini wavae na kitu gani na kipi hakiwafai. Ukiachana na kujua umbo lako ni muhimu pia kujua ni vitu gani si lazima kuwa navyo hata kama vinaendana na umbo lako.
Leo tunakuletea vitu vichache ambavyo huvihitaji na usimalize pesa yako kuvinunua.
- Kununua Mavazi Kwasababu Umeona Influencers Wamevaa
Kuna makampuni ambayo wanalipa influencers wavae mavazi yao, kila kona unayopita unakutana na hilo vazi, ukalipenda na kuamua ulinunue na wewe hata kama unajua au unaona kabisa hili vazi hutolivaa huko mbeleni, hakikisha unajua ku-control matamanio na nunua vazi endapo tu utaona utalivaa mara nyingi, kabla ua kunua hilo vazi jiulize maswali haya.
- Je nitalivaa hili vazi?
- Je linaendana na life style yako?
- Je linaendana na style zako nyingine za mavazi?
Kama maswali yote haya jibu lake ni hapana basi achana na vazi hilo.
- Epuka Edgy Trend
Kuna trend ambazo zipo bold yaani zile ambazo ziko tofauti kwamfano kwasasa kuna trend ya patchwork denim, jeans ambazo zina viraka viraka, kwasasa kila unapopita unakutana na mtu amevaa na inaonekana sawa kwasababu ipo kwenye trend, lakini umejiuliza miezi kadhaa mbele utaweza kuvaa tena hili vazi pale ambapo trend itakuwa imeisha? Kama ungependa kufuata trend hakikisha unanunua kitu ambacho hata trend ikipotea kinaweza kuvalika.

- Usinunue Mavazi On Sale Sababu Tu Yapo On Sale
Tunapenda ku-save pesa unakutana na vazi unaona bei rahisi basi unaamua kununua kuna neno wahenga walisema “bure aghari” kuna sababu ya kwanini iko kitu kipo onsale kwanini hakija uzika, hakikisha hata kama umekutana na vazi au accessory zipo kwenye sale zinaendana na style yako. Unanunua kitu sababu tu bei rahisi lakini mbeleni hukitumii hata kama ni pesa ndogo umetumia bado inakuwa haina maana.

- Cheap Fabric
Hakuna kitu kina haribu muonekano kama cheap fabric, inawezekana umeona gauni zuri, style yako linakukaa vizuri mwilini lakini kama fabric yake ni mbaya achana nao, sio tu litakufanya uonekane cheap lakini pia linaweza kuharibika kwa urahisi.
Kununua Mavazi Yasiyo Endana Na Umbo Lako
Hiki ni muhimu sana unapoteza pesa unaponunua vazi ambalo haliendani na umbo lako, kwa maana hutolivaa na hata kama ukiwa kichwa ngumu ukavaa basi wengi watakuwa wanakushangaa na hautokuwa comfortable hakikisha unatumia pesa yako kwa kitu ambacho utavaa na kuwa comfortable nacho.
Kununua Fake
Inawezekana unapenda vitu vya brand fulani na hauna uwezo wa kununua, haimaanishi ununue fake yake, nunua kitu chenye quality hata kama sio brand kubwa lakini kiwe kizuri kuliko kupoteza pesa kwenye fake.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…