Kama kuna kitu tunakitupia macho kwasasa ni Wasafi festival, tunapenda kuona namna ambavyo wasanii wapo pamoja na kutupa ideas mbalimbali za mavazi. Ikiwa week hii festival hii inaelekea Sumbawanga tumeona wakiwa ndio wako safarini kuelekea sehemu husika tukaona sio mbaya kuleta hapa airport sytles zao na utuambie ya nani imekuvutia zaidi?
Diamond Platnumz, Darassa & Noel Gio wakiwa wamevalia hoodie na suruali wakiwa wamevalizia mionekano yao na miwani na accessories mbalimbali.

Mbosso, G Nako pamoja na Chegge hawa walichagua kuvaa jackets & sweater’s na suruali za jeans. Mbosso na Chegge walivalia kicks na kofia huku G nako yeye akiwa amechagua kuwa less kwa kutoku accessories na chochote bali attention yake alimalizia kwenye viatu aina ya boots zenye kisigino kirefu kidogo.

Tuliwaona Mzee Wa Bwax, Mr. Blue na J Melody wakiwa kwenye colorful looks ikiwa kila mmoja akiwa na style yake iliyompendeza kuvaa katika safari yake.

Alikuwepo pia Barnaba, Lil Ommy pamoja na Bill Nas, ambapo Barnaba yeye alikuwa amevalia t shirt nyekundu, jacket pamoja na suruali akamalizia na boots na accessories mbalimbali, Lil Ommy alikuwa na details mbalimbali kama kofia, scarf na miwani huku outfit yake ikiwa simple, Bill Nas yeye alichagua kuwa kwenye Denim on Denim amemalizia muonekano wake na kiccks, bandana na miwani.

Tuambie muonekano wa nani umekaa ki-airport zaidi kati ya hawa?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…