Kila kunapokucha mambo yanazidi kubaadilika, teknolojia inazidi kukua , wigo wa Sanaa ya mitindo unazidi nchini Tanzania na ulimwenguni kote kwani hakuna anaetaka kubaki nyuma katika ulimwengu wa mitindo .
Wabunifu nao wanazidi kushika hatamu kwa kubuni vitu mbalimbali ilimradi tu kuwafanya watu kuwa na muonekano tafauti tofauti.
AfroSwagga imefanya mahojiano na mmoja wa wabunifu wa mabaibui nchini Tanzania anaejuliakana kwa jina la Faryz nae alikua na haya ya kusema
AfroSwagga : Unauzungumziaje ulimwengu wa mitindo Tanzania?
Faryz: Kiukweli mitindo inazidi kupanuka kila siku kadri teknolojia inavyokua watu wanazidi kuelewa, kupenda na kujua umuhimu wamitindo katika maisha .
AfroSwagga : Kwanini uliamua kubuni mabaibui na sio kitu kingine?
Faryz: Sababu kubwa niliona vazi la baibui limechukuliwa kama vazi la msimu mfano wakati wa ramadhani lakini sivyo ivo baibui ni vazi unaloweza kuvaa mahali popote na wakati wowote, kwani ni vazi la stara linalokufanya kuwa huru mahali popote.
AfroSwagga : Wabunifu wengi wanabuni vitu kwa kuwalenga vijana Zaidi ni kwanini na kwanini wewe unaona uko tofauti?
Faryz: Kitu kikubwa ambacho wengi wanaangalia ni soko, vijana ndio kundi kubwa la watu wanaopenda kwenda na mitindo kuliko watu wengine ndio maana wengi wanawaangalia vijana Zaidi lakini mimi niko tofauti kwani baibui halichagui umri mtu yoyote anaweza kuvaa baibui.
AfroSwagga: Changamoto gani ambazo unakutana nazo katika kazi yako ya ubunifu?
Faryz : Changamoto kubwa ambayo nakutana nayo mimi kama mimi ni ukosefu wa malighafi hapa nchini , kwani mimi natumia mabaibui ya mitumba nabuni tofauti lakini watu wanayapenda,
AfroSwagga: Onesho la Mitindo liliyofanyika jumamosi ya tar13 ( stara)lengo la kuandaa onesho hilo lilikua ni nini, na kwanini mkaipa jina la stara?
Faryz : kwanza sababu iliyofanya tuipe jina na stara ni kwa sababu baibui ni vazi la stara na lengo la onesho ilikua ni kuwakumbusha watu hasa wanawake kujistiri sio kipindi tu cha ramadhani ila muda wote watu wakumbuke kujistiri
AfroSwagga : unatoa ushauri gani kwa wabunifu wadogo ambao wanatamani kufanya kazi hii lakini hawajui wapi pa kuanzia
Faryz: Kitu chakuzingatia nikujiamini na kuipenda kazi yako, pia watumie mitandao ya kijamii kujitangaza watafika mbali na kutimiza malengo yao , mimi ni mitandao ya kijamii iliyonisaidia kujitangaza na kutangaza kazi yangu.
AfroSwagga: Unatoa ushauri gani kwa jamii
Faryz: Jamii ichukulie mitindo kama sehemu ya maisha na pia wasiruhusu mitindo kuharibu mila na desturi za Tanzania nawasihi sana wanawake wakumbuke kujistiri ili kujilindia heshima katika jamii.
JIONEE UBUNIFU WAKE KATIKA PICHA
Kwa Picha zaidi unaweza kutembelea ukurasa wake wa Instagram @my_hijjab_my_stara
Related posts
2 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More Information here to that Topic: afroswagga.com/mitindo/baibui-vazi-la-stara/ […]
… [Trackback]
[…] There you can find 98794 additional Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/baibui-vazi-la-stara/ […]