Mwaka 2018 umeweza kuwa wa mafanikio makubwa mabapo tumeona tasnia ya urembo, mitindo na ubunifu ikizidi sogea mbele. Twaweza sema hapa tulipo si sawa na miaka 5 nyuma na hakika tujipongeze kwa hili.
Tasnia ya urembo, mitindo na ubunifu yawakutanisha watu wengi wakiwemo wabunifu wa mavazi, make-up artists, photographers, stylists, models, bloggers, style influencers, wanasanii iwe muziki ama filamu na wengine wengi. Kila mmoja hapa ana mchango wake nasi Afroswagga tungependa kutoa rai kwa ila muhusika.
- Wasanii
Hasa katika tasnia ya muziki ambayo inakuwa kwa kasi sana na kuangaliwa sana na mataifa mbalimbali, tungependa kuona wabunifu nchini wakitumiwa katika kazi zenu kwa wingi. Wasanii wengi wakipendelea kuvaa mavazi toka nje na mengi yakiwa feki huku kuna wabunifu nchini ambao wangeweza fanya zaidi katika kazi zao.
KUNA UMUHIMU WA WASANII KUWA NA WABUNIFU WAO?
- Stylist
Tulizungumzia wasanii kuwatumia stylists katika kazi zao na hiki tumeona wengi wakilifanyia kazi lakini pale stylists wanapotumika hatuoni tofauti na wengi wao huendelea kuwavalisha wasanii nguo zile zile, creativity na style personality inakosekana, tungependa mwaka huu tuone tofauti tupate ladha tofauti hii italeta ushindani na chachu ya stylist kufikiria wafanye nini kutoka nje ya box na kuwafanya watu maarufu wawe na mionekano ya kipekee na mizuri.
BADO TUNAHITAJI MA STYLIST KATIKA VIDEO SHOOTING
- Style Influencers
Fashionstas wengi nchini wana uwezo wa kuwainspire Watanzania wengi katika suala la mavazi. Wengi wetu, ambao tumhepedeza pendeza pia twaishia kulike tu picha. Tutapendelea tukiona watanzania wengi wakipendezwa na kukoshwa na kazi za style and fashion influencers wetu ambapo mtanzania wa kawaida naye aweze ona na kusema name naweza pendeza kama fulani akitumia nguo zake ziwe mtumba ama dukani, lakini pia kutoa tips now and then ili wa Tanzania wapate kujifunza kutoka kwenu pia, lets make Tanzania Fashionable.
- Wabunifu
Hakika twaendelea jivunia wabunifu wengi wakubwa kwa wachanga tulionao katik fani hii. Ni kazi nzuri yafanyika. Lakini twaomba kwa wachache wanaokosea kujirekebisha hasa katika crearivity maana wengi walalamikiwa kuwa sio wabunifu bali wacopy mishono toka nchi nyingine. Tungependa kuona Made In Tanzania kweli ambapo hata mastaa toka nchi nyingine wataweza vaa kazi zenu. Creativity ianzie toka uchaguzi wa materials and fabrics, designs, mishono, finishing na hata adveristing of the brand.
Tunatengeneza Aina Gani Ya Kizazi Cha Wabunifu Wa Baadae?
- Photographers Na Makeup Artist
Kazi nzuri sana yafanywa na makeup artists na wapicha picha wakishirikiana na wabunifu lakini pale kitu chochote kinapozidi, hupoteza uhalisia. Edits za kupita kiasi hadi nguo na ngozi ikibadilika tuache hizi mambo. Pia makeup zisizoendana na tukio nazo twaomba zibaki 2018.
2018 ilikuwa nzuri, 2019 tuipaishe bendera ya nchi yetu kupitia fashion & beauty mbali zaidi.
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Here you will find 39888 more Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/barua-ya-kufunga-na-kufungua-mwaka-kwa-wapenzi-wa-afroswagga/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/barua-ya-kufunga-na-kufungua-mwaka-kwa-wapenzi-wa-afroswagga/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/barua-ya-kufunga-na-kufungua-mwaka-kwa-wapenzi-wa-afroswagga/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/mitindo/barua-ya-kufunga-na-kufungua-mwaka-kwa-wapenzi-wa-afroswagga/ […]