We love when a designer steps outside the box, mara nyingi wabunifu wakitoa collection zao hawajisumbui kufanya vitu vingine kuendelea kutangaza collection zao hizo. Fashion Campaign ni namna mojawapo ambayo inamuwezesha mbunifu kutangaza collection yake, zipo namna mbalimbali za kufanya campaign hizi, kwa kuchagua aina gani ya watu ungependa kuwagusa na bidhaa yako kupita campaign yako hio.
Bijoux yeye amechagua kusheherekea utamaduni, Bijoux na team yake walisafiri mpaka singida & bagamoyo ku-shoot hii campaign ( the effort). Tumependa kwamba ameweza kuonyesha sio tu wadada na wamama wa mjini wanaweza kuvaa hizi nguo bali hata wale ambapo wapo vijijini wanaweza kuvaa. Na kwamba mavazi yake anayotengeneza yanaweza kuvaliwa na yoyote.
Bijoux hakwenda na models Singida bali walitumia watu wa kawaida, kwa mujibu wa Bijoux models wake hawa walikuwa ni baadhi ya ndugu wa stylist Vaazi ambae ndiye alikuwa art director kwenye campaign hio.
Lakini pia tumependa kwamba hawakwenda sehemu fancy sio kama vile ambavyo tumezoea kuona photo shoots nyingi zikifanyika, walienda kijijini na walionyesha mavazi yakiwa yamevaliwa nyumbani huku models hawa wakiwa wanafanya shughuli zao za kawaida kama kusukana, kusuka ukili, kutwanga etc.
Hii campaign imebeba uhalisia wetu na utamaduni wetu, tumependa tulichokiona na tunatamani kuona zaidi ya hivi kwa wabunifu wengine.
Art director #vaazi_stylist
Designer #bijou
Sniper #Kevoo
Location #bagamoyo / #Singida
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…