Familia ya mwanamuziki Diamond Platnumz ndio familia ambayo inaongoza kwa kufuatiliwa kwa sasa Africa Mashariki na hii inatokana na visanga vyao vya kila siku, kwa kuliona hilo wenyewe wameamua kukuleta maisha yao karibu na wewe, Well wametoa Teaser ya reality show yao ambayo inaitwa ” The Real Life Of Wasafi (TRLOW)”
Kwetu tulikuwa tunasubiria teaser itoke kwa maana teaser ndio hubeba kila kitu kama itakupa hamasa ya kuangalia au lah, kwenye teaser hii tumeangalia sana outfit zilizopo nini kilikuwa nyuma ya hizi outfits tumemuuliza stylist wa Teaser hii ambae ni Noel Ndale amesema theme ilikuwa “BLACK ROYAL EXCELLENCE”
Tulivyo iona hii teaser kwa mara ya kwanza haraka haraka ikatujia image ya Coming To America, kwa wanaume suit walizo vaa na namna wame zi-accessorize kichwani ikatujia taswira ya movie ya Coming To America ya Eddie Murphy ambayo ilitoka mwaka 1988,
ukimuangalia Malomboso na Lavalava walivyo valishwa utaelewa tunaongelea nini
Esma yeye amepewa mavazi ya miaka ya miaka ya 1940 – 1960 ambapo wanawake walikuwa wanavaa magauni ya cinderella na gloves mikononi ilikuwa ni wanawake wachache sana wa ki-Africa ambao wanavalishwa hivi hasa wale wenye hadhi fulani katika jamii, lakini pia walikuwa wakivaa kwenye sherehe.
Kwa Queen Darleen, Diamond na walio baki style zao zipo kisasa zaidi, sana sana walicho ongezewa ni accessories ambazo zimekaa ni “royal”.
View this post on InstagramThe Real Life Of Wasafi #TRLOW 📺 …Coming soon On @wasafitv
A post shared by Wasafi TV (@wasafitv) on
Tumependa fashion namna wamejaribu kufanya ionekane tofauti na teaser nyingine, lakini tungefurahi zaidi kama kungekuwa na fusion, yaani kuchanganya theme lakini zote zika blend in na sio kila moja kusimama kivyake, kama ambavyo unaona ukiwakeka Mboso na Lavalava unapata kitu cha tofauti, Diamond na Mose wakisimama wanaleta theme nyingine, Esma peke yake, mama Diamond, Romy, Harmonize Na Rayvanny wana theme nyingine.
All in all wamejaribu na we cant wait kuona nini kinakuja.
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…