Huwa tunachukua muda kukosoa tunapoona makosa lakini pia huwa hatuachi kusifia pale panapo stahiki sifa, Miaka michache nyuma tulishawahi kukosoa bongo movies kutokana na makosa mbalimbali ya fashion leo tupo hapa kutoa pongezi kwao.
Hatujui kama walisoma au ni kwenda na wakati kwasasa bongo movies wanajitahidi sana katika swala la mitindo, wanavaa kutokana na sehemu walipo, tunapenda kuona kwenye sherehe wanavaa kama sherehe, kazini wanavaa kama kazini tumepiga hatua kutoka pale ambapo tulikua.
Makeup na nywele, kukumbuka tu nywele na makeup za miaka ya nyuma utaona namna ambavyo kuna tofauti sana sana kwasasa wengi wanajitahidi kupaka makeup nzuri na kusuka nywele zenye kupendeza.

Tumependa kwamba sasa hivi wanatilia mkazo mionekano yao kwenye movies na hivi ndivyo tunatakiwa kuwa na kupiga hatua zaidi, kuona tumeacha kuvaa kama vikatuni inatia moyo zamani ilikuwa vazi la club unakuta actress kavaa kazini, nywele imesimama ina rangi ya kazini mdada kasuka na ndio reception wa ofisini au makeup ya kwendea harusini yupo ofisini.

Sasa hivi tunaona mavazi, nywele, viatu unaenda na uhusika na mahali alipo muigizaji, tunapenda namna ambavyo mnawekeza katika swala la mionekano, Tuendelee hivihivi ata movies zetu zikionyeshwa nje wajue tupo serious.
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…