Kwa namna ambavyo Dunia inaenda sasa watu wengi wanawake kwa wanaume hawajali namna ambavyo wanaonekana, unaweza kusema mbona sasa hivi ndio watu wanajali mionekano tunaweza kusema ni watu wachache sana wanaangalia wanachovaa, wengi tunavaa tu ilimradi tuvae, unaweza kukuta mtu amevaa nguo za gym akiwa anafanya shopping au matembezini, unaweza kukutana na mtu kavaa viatu vya kutembelea ndani nje, yes tunavaa lakini hatujali namna ambavyo tunaonekana au kama hilo vazi linafaa sehemu uendayo.
Kwasababu hizi ukivaa vyema basi una stand out na kuwa wa tofauti kama ambavyo kuna msemo unasema “in the world full of Kardashian be the Beyonce”, Je kunafaida gani za ku-stand out na kuwa classy / elegant?
- Unaongeza Kujiamini
Unapovaa vyema kutokana na mazingira, unachoenda kufanya basi unakuwa unajiamini zaidi na kuweza kufikia malengo yako na zaidi kuliko ukiwa umevaa hovyo utaanza kujishtukia na kupunguza kujiamini kwako.
- Kupata Fursa Nyingi Zaidi
Kwasababu unajiamini basi wengine pia watakuamini na kukupa nafasi zile ambazo nyingine hata hukuzitegemea, unaweza kuona haya hasa pale kinapotokea kitu kwa mtu ambae anapendeza watu wanasema mbona hafananii na muonekano wake? Hii ni kwamba watu wanaamini katika mionekano zaidi.

- Kuheshimiwa / Kutendewa Vizuri
Kama tulivyosema hapo juu unapovaa vyema unaaminika zaidi na watu wata ku-treat vizuri kutokana tu na namna ambavyo umejionyesha kwao, hata barabarani wengi wakikuta umevaa suit au umependeza watakuita boss wakati ukiwa hovyo hakuna ambae atajisumbua na wewe.
Well jaribu kubadilika na kupendeza kisha utuambie ni namna gani huko kwenye matembezi yako wamekupokea.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…