Miaka ya nyuma watu wenye miile minene walikuwa wanapata sana shida kujua wavae nini na wavaeje, ilikuwa shida zaidi kwa maana nguo nyingi zilikuwa zina buniwa kwa ajili ya watu wenye miili midogo lakini kwa sasa dunia imebadilika na wao wanapata mavazi yao na hata kushirikishwa katika runways, Plus size & slaying.
Leo tumeona tuwaletee fashion tips tatu ambazo zinaweza kukusaidia kama una mwili mkubwa (mnene)
Highlight zile feature zako nzuri – watu wengi wenge miili mikubwa huwa wanakosea kwa kuvaa vitu kama ambavyo wanavyo vaa watu wenye miili midogo mf: mtu mwele mwili mdogo anaweza kuvaa gauni na belt akafungia belt tumboni, yes anaweza sababu tumbo lake ni dogo lakini kam wewe ni mnene na unatumbo kubwa hupashwi kuvalia mkanda hapo, valia mkanda juu ya kiuno au chini kidogo ya matiti hii itasaidia sio tu kuficha tumbo lako bali pia kuonyesha shape yako vizuri.
Usione aibu kuonyesha mwili wako – hili ni tatizo ambalo wengi wanalo utakuta mtu ambae ni plus size anavaa nguo kubwa ndefu,ukimuuliza kwanini atasema labda nina mikono minene au nina miguu minene bila kujua kama anaweza kuonyesha hizo sehemu na akapendeza tu bila ya tatizo.
Cheza na pattern – wengi huwa tunavaa nguo nyeusi (hii inasemekana ina saidia kukufanya uonekane mwembamba) achana na hio dhana jua kucheza na pattern na utashangaa jinsi ambavyo unaweza kuvaa rangi lakini pia ukapendeza na huo huo mwili wako.
Mwisho jipenda na kuwa na confidence kwamba your beautiful the way you are. kusoma tips nyingine unaweza ku click hapa.
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…