Viatu virefu sio ufunguo wa vazi kuonekana classy na elegant,inawezekana ukavaa viatu virefu vizuri lakini bado ukaonekana messy, inawezekana ukawa umekosea kwenye mavazi au accessories zako, cha muhimu katika kuchagua mavazi na viatu ni kuangalia kipi kinaendana na kipi.
Kuna aina viatu ambavyo hutoa vibe ya casual look ambapo wengi tunaamini viatu kama sneakers, sandals, flats zinafanya muonekano uonekane casual na sio elegant, lakini kumbe unaweza kuvaa aina hio ya viatu na bado muonekano wako ukawa elegant, unachohitaji ni kujua namna ya kuufanya muonekano wako uonekane katika hali nzuri.
Mfano mzuri ni uchaguzi wa viatu hivyo kama ni mpenzi wa flats basi nunua ambazo zina rangi na design nzuri, huwezi kuvaa sandals ina midoll au rangi kali na vazi la maana na ukanonekana vyema lazima viatu vitashusha vazi hilo, sio kwasababu ni sandals bali ni design na uchaguzi wa rangi za viatu hivyo.
Leo tupo na mwanamitindo na fashionista Julitha Kabete ambae tumemuona mara nyingi akiwa amevalia flat sandals na kuonekana amependeza
kama unaenda sehemu za ufukweni au sehemu za ku-swim basi unaweza kuvaa piecez zako nzuri uka style vyema na ukavaa flats zako kama Julitha hapo chini

Kwa wale wa casual outings kwenda movies, running errands au shopping kwenye basi unaweza kuvaa suruali yako iwe jeans au material yoyote na ukamalizia muonekano wako na flats.

Kwa mitoko muhimu kiasi kama kwenda kula lunch, brunch, dinner za kawaida na marafiki unaweza kuvaa vazi lako linaloendana na sehemu unayoenda na ukamalizia muonekano na flats zako.

Well kikubwa kuhusu kuvaa flats ni kuhakikisha miguu yako misafi, umepaka mafuta vyema na kucha ziwe safi lakini pia hakikisha flats zako zinaendana na mavazi yako.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…