Inawezekana una mavazi machache au unayo mengi lakini unapenda kurudia mavazi yako, ikiwa Dunia inatupelekesha kuamini kwamba kurudia nguo ni jambo la ajabu tupo hapa kukwambia ni sawa kurudia nguo, Lakini je unazirudiaje ili watu wasijue kama umezirudia? Leo tunakuletea tips chache za nini ufanye kurudia vazi lako na usijulikane
Kuwa mbunifu na combination zako
Kama unavaa vazi moja kilasiku na viatu vilevile, mkufu uleule, handbag ileile ni rahisi kugundulika kwamba umerudia vazi lako, jaribu kubadilisha combination zako mara kwa mara. Mfano una floral shirt ina maua mekundu, kijani na nyeupe basi jua unaweza kuvalia suruali za rangi hizo na hio blouse usivae na rangi ya kijani kila mara, unaweza kuvaa nyeusi, unaweza kuvaa nyekundu au nyeupe na hapo utakuwa umeweza kurudia nguo yako bila ya watu ku-notice.

Badilisha Style Ya Nywele
Unaweza ukawa unajaaribu kila siku kumix your outfit na ukawa unaonekana unarudia nguo kila siku. sio mbaya kitu cha muhimu unachotakiwa kufanya ni kujitaidi kubadilisha muonekano wa nywele zako unaweza kucheza na nywele zako jinsi unavyotaka mara leo umebana, kesho umeachia itakusaidia uonekane mtu unayebadilika kila siku hata kama ukiwa unarudia nguo.
Jaribu Kuvaa Accessories
Hiki ni kitu cha muhimu sana kama mtu wa kurudia sana nguo basi jaribu kuongezea accessory kwa sababu zitawafanya watu wazingatie sana accessory zako na kutofocus na outfit. kitu cha muhimu ni kuadd accessory but keep jewely simple yani usiweke vitu vingi, add accessory ambazo zitakufanya uonekane smart unaweza ukaadd earing, bracelet, necklace.
Layering is everything
unaambiwa hivi layering is an art na kama unavyojua hakuna art ambayo haina faida. kitendo cha kuongezea shirt, scarf, sweater katika outfit yako itakufanya ubadilishe kabisa muonekano wako na kukufanya uwe perfect,kama unampongo wa kurudia outfit yako basi jitaidi sana kufanya layering.

Badilisha Handbags
jitaidi sana kubadilisha hangbag yako itakufanya usionekane unarudia outfit. ukiwa na mikoba mingi basi itakufanya uwe na choice nyingi kama unaweza basi jitadi sana kila ukichange handbag iwe inaendana na kitu kimoja kwenye outfit yako.
Badilisha Viatu
haijalishi umevaa same outfit mara ngapi lakini ukijitaidi kubadilisha kiatu chako katika hiyo outfits itakufanya uonekane mpya. kitendo cha kubadilisha kiatu kitakufanya ubadilishe muonekano wote na wataalamu wa mambo ya mitindo wanakuambia kila siku (the shoe closes your appearance) so jitaidi kubadilisha kiatu itakufanya uonekane tofauti kama ulikuwa unavalia mules unaweza ukachange ukaanza kuvaa na high heels au flats.

Know Your Audience
najua unaweza ukawa unapenda kurepeat outfit kwa sababu unaambiwaga unapendeza sana but cha muhimu ni kujua audience yako ni watu wa aina gani kama umevaa kwenye birthday party basi usivae tena kwa watu wa aina iyo jitaidi sana ukavae katika different place hii itakufanya usionekane unarudia nguo.
Note; ukiona unashinda kufanya hivyo vyote basi usisumbuke sana unaweza kuadd jacket na itakufanya usiwe noticed. kurudia nguo sio vibaya ila kushindwa kustyle outfit yako ndio kitu kibaya ni matumaini yetu umetuelewa na itakusaidia katika kubadilisha muonekano wako.
imeandikwa na @gotchathegreatest
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…