Katika kutafuta jibu la malalamiko ya wengi kwamba wabunifu siku hizi wanaigiana kazi na kwamba kwa sasa wabunifu hakuna kuna ma fundi cherehani ili bidi tuhoji pande zote mbili kwa wadada na wakaka, tumesha ona majibu ya Martin Kadinda na samuel zebedayo lakini je wadada wao wana maoni gani na hawa ni Kiara Sheba Na Husna Tandika na maoni yao kuhusu swala hilo
Afroswagga: Dada Husna wewe una liongeleaje hili swala la wa Tanzania kusema ” Tanzania hamna wabunifu bali kuna mafundi cherehani”
Husna Tandika : Kuhusu fundi Cherehani ilo sijaelewa kwanini wanasema hivyo, maana nnavyojua wabunifu wengi hawajuagi kushona. Rather wako karibu na mafundi but sio washonaji
Afroswagga: Vipi Kuhusu kuigana kazi?
Husna Tandika: Ni kweli wengi wanaigizana sana kazi, na mara nyingi sana inatokea kutokana na wateja wengi wanapenda kuvaa nguo ambayo imevaliwa na star. Then kila mtu atataka that look.
I once mvisha jokate, nilipata wateja wengi mno ambao walitaka kuvaa kama nguo yake… Baadhi yao without even knowing was my design
Pia unakuta wateja wengi wanakuja kwa mbunifu wakiwa na picha zao. As in “nataka unishonee kama lulu, au nataka unishonee kama Wema / Mobetto nk”
So ni mawili either ufanye anachotaka mteja au umpe ushauri na ubuni wewe kitu kingine au similar but unaweka kitu cha kufanya brand yako ijulikane
But just kumalizia ni kwamba mbunifu anafanya more than one job kuliko kukaa na kubuni nguo. Yeye ni marketing, hr, mshauri, accountant etc. Reason why wengi wanakosa ile creative mode.
Lakini pia tulifanya mahojiano na mbunifu Kiara Sheba na yeye alikuwa na haya ya kusema
Kiara Sheba: Wabunifu wapo.Kinachofanya watu waseme kua hamna wabunifu ni mafundi cherehani kujiita wabunifu bila kuzingatia vigezo vya ubunifu. Kibongobongo pia ubunifu unachukuliwa poa, inaonekana ni fani ambayo mtu yeyote anaweza fanya.Lakini kiukweli ubunifu ni fani ya kuumiza kichwa sana ili kupata mawazo mapya na mitindo mipya.
Kuhusu kuigana kazi..Kiukweli kuna ukweli uliopo kwenye hilo. Ukizingatia fundi cherehani wengi wanajiita wabunifu. Na kwa kuwa hawana ubunifu kunakua na copy paste nyingi. Hii inarahisishwa na utandawazi, kila kitu kipo mitandaoni kwahio kudesa ni rahisi mno. Lakini pia kuna kitu wenye ubunifu kinaitwa misimu. Misimu inakua na rangi na mitindo inayofanana, kwa mfano sahivi mitindo ya miaka ya 80 iko kwenye fashion kwahio unakuta wabunifu wanabuni nguo wakiwa na hilo kichwani.
Kwahio sa zingine sio kuigana ni kufuata trends
Related posts
2 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/mitindo/husna-tandika-kiara-sheba-ni-kweli-wabunifu-wanaigiana-kazi/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/mitindo/husna-tandika-kiara-sheba-ni-kweli-wabunifu-wanaigiana-kazi/ […]