Tuko hapa tukiangalia namna ambavyo wabunifu kutoka Nchi za Africa yaani majirani zetu wakiwavalisha watu maarufu wakubwa wenye influence kubwa Duniani, wakati sisi tukiendelea kuwa ndugu watizamaji. Kama ulikuwa hujui basi ngoja tukujuze, mwaka huu umekuwa na revolution kubwa kwa watu maarufu kutoa support kwa wabunifu wadogo na wakubwa kutoka Africa, kuna movement ambazo zipo kama #wearafricadesigns au #buyblackowned na hii ni kutokana kuonekana wa-Africa kuto kutoa support kwa wa-Africa wenzao na kupelekea kutajirisha wengine huku wakiwaacha ndugu zao wakiendelea kusota na kunyanyika.
Hii imeonekana sio tu katika vyakula na mambo mengine lakini hata katika fashion pia, seems like everybody is woke na kila mtu anataka mwingine nae anyanyuke, Nchi nyingi zimefanikiwa na movement hii, from Nigeria,Senegal, Cameroon, South Africa na kwingineko ,
Katika event kubwa ya global citizen festival katika mavazi yake mwanamziki Beyonce katika mionekano yake alichagua kuvalishwa na wabunifu wadogo kutoka Africa ambapo usiku ule akiwa ana perform alivaa green outfit kutoka kwa South Africa Fashion brandEnhle Mbali Maphumulo and Quiteria & George collaboration, Kama tungekuta hii design kwenye duka definitely tunge shout a Beyonce look, that embellished body suit, and extra designed cover up was a statement of the outfit.
Hivi karibuni tumemuona mwanamuziki na muigizaji Kelly Rowland ambae alikuwa kundi moja na Beyonce “Destiny’s Child” akiwa amepost picha katika instagram yake akiwa amevalia yellow & blue two pieces za kitenge kutoka kwa mbunifu Tehilah Abakasanga kutoka brand iitwayo ÖFUURË inayotoka Nchini Nigeria, she paired her look with statement earrings & box braids, like a true African woman
Mwanamitindo Tyra Banks na yeye tumemuona akiwa amepost hii picha katika Instagram yake akiwa amevalia kitenge top kutoka kwa brand ya UberStyle Woman kutoka Nigeria,
Lakini pia katikati ya mwaka huu tulimuona mbunifu Claude Lavie Kameni Kutoka Cameroon Alivyoweza Kumvalisha Janet Jackson Na Tracee Ellis Ross, Wakati Janet alimvalisha katika video ya wimbo wake mpya wa Made For Now ambapo wimbo huu ulikuwa kama kurudi kwake katika game baada ya kuolewa, na kujifungua, ilikuwa ni big deal sio tu kumvalisha Janet bali kumvalisha kwa kipindi muhimu kama icho na to think that video itaendelea kuishi milele
Lakini pia aliweza kumvalisha mchekeshaji na muigizaji Tracee Ellis Ross katika American Music Awards na Tracee alikuwa host wa siku hio, ambapo aliamua kuvaa design za wabunifu weusi na Lavie alikuwa mmoja wao
Ni matumaini yetu tutamuona msanii mkubwa akiwa amevalia product kutoka kwa wabunifu kutoka Tanzania
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Information here to that Topic: afroswagga.com/mitindo/its-african-designers-time-from-beyonce-janet-jackson-tyra-bank-and-many-more/ […]