Kubadilisha sidiria yako mara kwa mara ni njia mojawapo ya kuepuka hatari za kuvaa sidiria isiyofaa/kukutosha, ambayo inaweza kukuletea athari za maumivu ya kichwa na maumivu ya mgongo kutokana na poor posture ya sidiria hio.
Kutokana na uchunguzi wa Harper Wilde, 70% ya wanawake walisema sidiria hukaa au kuvaa sidiria kati ya miaka miwili hadi mitano. Makala hii inaelezea kwa nini, jinsi gani, na wakati wa kubadilisha sidiria yako uipendayo na kununua nyingine.
- Kwa nini huwezi kuvaa Sidiria moja milele?
Sidiria hutengenezwa kwa material ya kuvutika ambayo husaidia kutoa support kwa namna moja au nyingine, Sidiria lazima iweze kusogea na kujikunja kutokana na mwili unavyopelekwa, pamoja na kuyaweka matiti katika hali nzuri. Elastic inayowekwa kwenye sidiria inaruhusu hii kutokea, lakini sidiria inapoteza ufanisi na muonekano wake mara baada ya matumizi mengi, kama kufuliwa au kuvaliwa mara kwa mara, huchoka na hivyo hulegea na kupoteza ufanisi, pia kupungua au kuongezeka mwili kuna weza kusababisha upaswe kununua sidiria nyingine.

- Ni mara ngapi unapaswa kubadilisha sidiria yako?
Hili ni swali rahisi, lakini jibu linaweza kuwa gumu kulingana na mara ngapi unatumia na kuosha/kufua sidiria yako, pamoja na ni kiasi mwili wako unabadilika. Hata kwa matumizi ya uchache na uangalifu, sidiria zote zitapoteza umbo lake baada ya muda kadiri nyuzi za elastic kwenye bendi na kamba zinavyoharibika.
Utafiti unapendekeza ubadilishe / kununua sidiria kila baada miezi 6-9, lakini inaaminika kuwa ikitumika kwa uangalifu sahihi, sidiria yako inapaswa kudumu muda mrefu zaidi.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…