Leo kwenye pitapita zetu huko mitandaoni tukakutana na hii video ya mwanadada kutoka Nigeria ambae anasema amekutana na mchepuko wa mume wake na aka-realize tatizo ni yeye.
Ukiendelea kusikiliza hii video anasema kwamba huyo mchepuko ni fine girl, anavyovaa, nywele zake na anavyojijali wakati yeye ana nywele zake za minyoosho toka January.
Well tulivyoona hii video ikatufanya tuwaze je ni sawa kujiachia kutokujijali sababu tu umeshaolewa yaani siku ya mwisho mwanaume kakuona umependeza ni siku yenu ya harusi baada ya hapo wewe na vijora vijora na wewe, na je ni sawa mwanaume kuto nje na kucheat kisa tu mwanamke wake kaacha kujijali? Kwanini asimwambie ajijali?
well tunadhani hiki kitu kinaenda both ways, kwa mwanamke na mwanaume pia
Inatakiwa tujue kwamba kuolewa hakubadilishi kitu ni kwamba umetoka kuwa single na sasa umeolewa, huitaji kubadilisha dressing code wala kuacha kujipenda, dressing up sio kwaajili ya mtu bali pia ni kwaajili yetu, kama zamani ulikuwa unajipenda ukamvutia mwanaume akuoe kwanini sasa hivi unajitupa? kwamba ulikuwa unavaa kuvutia mume na umeshampata inatosha?
Hata kama ni mke au mama unahitaji kuonekana vyema kwaajili yako mwenyewe, mume wako na watoto, chukua muda wako kusuka, kutengeneza kucha, dress up hata kama huendi mahali, nguo zako za kushindia ziwe safi.
As kwa mwanaume tunadhani alikuwa na uwezo wa kumwambia mkewe kabadilika na anaanza kupoteza mvuto kwake pretty sure mke angejitahidi kurekebisha tatizo lake.
Well let us know unafikiriaje kuhusu ili swala?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…