Katika msimu huu wa ramadhani, vazi lilokubwa na linalovaliwa na wanawake tulio wengi ni baibui, leo nataka tuangalie namna ambavyo tunaweza kuvaa mabaibui yetu kwa kuongezea baadhi ya vikorombwezo ili kulipa mwonekano wa tofauti machoni pa watazamaji wetu.
Baibui si vazi ambalo wengi wanalivaa kwa kuongeza vikolombwezo vingine, lakini nakuhakikishia ukiongeza baadhi ya vikolombwezo ambavyo ntakwenda kuvijadili leo utapata mwonekano wa kipekee na hautapoteza maana ya Stara
Kitu cha kuzingatia kwanza ni kwamba una baibu la aina gani na mtengenezaji wake ameliwekea urembo kiasi gani, ili usipoteze mvuto wa asili wa baibui lako, Hapa namaanisha kwamba unaweza ukawa tayari una baibu ambalo lina urembo wa kutosha hivyo si lazima kuliongezea, unaweza ukaongeza na kulifanya lipoteze mvuto.
Lakini pia unaweza ukawa na baibui ambalo halina urembo kabisa je nini ufanye ili kulitia nakshi?
Moja Unaweza ukavaa Baibui lako na juu ukavalia mkufu , si kweli kwamba ukivaa vazi hili huwezi kuvaa mkufu, ila ni kwamba utawezaje, wengi wetu tumezoea kuvaa mikufu kwa ndani ya blauzi, Unaweza ukavaa baibu lako kama kawaida na kisha ukavaa mkufu wako kwa nje, hio ndio moja wapo ya kuvaa baibui na mkufu, kama picha hapo juu inavyoonyesha.
Lakini pia unaweza endelea kubadili mwonekano wa baibui lako kwa kuvaa mkanda wa tumboni, na ni vema ukipata mkanda mpana ila si vema ukakubana sana, vingatia hapa unaweza ukavaa mkanda unaofanana na rangi ya viatu au mkoba na hata mtandio
Related posts
1 Comment
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/mitindo/jinsi-mkufu-na-makanda-unavyo-badilisha-mwonekano/ […]