Umeshawahi Kujiuliza Kwanini Ni Wewe Mwenyewe Unaenda Madukani Kununua Nguo Kisha Unakuwa Na Kabati Lina Mavazi Mengi Na Huyapendi? Inashangaza Right? Well Hii Hutakona Na Kwamba
- Unanunua Vitu Vilivyo Kwende Trend Kwa Wakati Fulani
Wengi huwa hatununui mavazi ambayo ni timeless tunaangalia nini kina trend kwa wakati huo na ndio hichohicho tunanunua na kuvaa mwisho wa siku trend inaisha tunabakia kuwa na mavazi mengi kabatini ambayo hatuyavai na hatuyapendi tena.
- Unanunua Kwasababu Umemuona Fulani Kavaa Na Kapendeza
Unaweza kumuona mtu maarufu au jirani yako kavaa vazi akapendeza na wewe ukaenda kununua kama hilo, mwisho wake unalivaa mara chache na kuona halifai tena unaliacha na kurukia vazi lingine. Lakini kumbe ukikaa ukajisikiliza na kujua wewe binafsi unapenda mavazi ya aina gani basi ungekua na kabati limejaa mavazi uyapendayo.
- Unanunua Ukidhani Utapungua Au Utanenepa Na Zitakutosha
Wangapi tupo guilty na hili? lol unanunua vazi kwasababu tu umeanza diet au gym ukijua utakonda au kwasababu umeanza kula unajua utanenepa unanunua vazi ili ukipungua au ukanenepa ulivae mwisho wa siku mwili unakugomea unabaki kuliangalia tu lile vazi kabatini na misonyo ya kujilaumu kwanini umenunua. Instead nunua mavazi kutokana na hali uliyonayo wakati huo incase ukinenepa au kupungua utafanya shopping upya.
- Unanunua Bila Kupangilia Au Kufikiria Kuhusu Vile Ulivyonavyo Tayari
Unaweza kujikuta na mavazi aina moja yamejirudia mara nyingi kabati kwako au ukaijikuta vazi fulani linaendana na nguo fulani tu huwezi kuvaa na nyingine hii ni kwasababu hatufikirii vile vilivyopo tayari, mfano ukinunua shirt waza utalivaa na suruali gani kabatini kwako na je kuna vazi lingine ambalo utaweza kuvalia hio shirt tena?
Makabati Yetu Yanapaswa Ku-reflect Maisha Yetu Inatakiwa Tujisikie Vizuri Tunapovaa
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you will find 87930 additional Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/kwanini-tunanunua-nguo-na-kuishia-na-mavazi-tusiyoyapenda/ […]