Marin Kadinda ni moja kati ya wabunifu wakubwa kabisa Tanzania, Kajipatia jina kubwa kupitia kazi yake ya ubunifu lakini je hili swala la wa Tanzania kulalamikia kazi zao na kusema “hamna wabunifu kuna mafundi cherehani” na kwamba “wabunifu Tanzania wana igiziana kazi zao” yeye ana liongeleaje?
Afroswagga: Martin kama mbunifu ambae ume tumia nguvu na kipaji chako cha ubunifu kufika hapa ulipo leo halafu una sikia kwamba wa Tanzania wanasema siku hizi hakuna wabunifu kuna mafundi cherehani una onaje au kuliongeleaje hili?
Martin: Kwasasa tanzania hakuna wabunifu kuna mafundi cherehani..? Kwanza kabisa ubunifu ni uwanja mkubwa sana ambapo kwa macho ya kawaida huwezi kuona.. fundi kuweka kushona mitindo mbali mbali hakumfanyi kuwa mbunifu.. uwezo kwa kubuni mchanganyiko mpya wa vitambaa.. vifungo.. zipu na malighafi mengine katika kazi ya ushonaji ndo kunakufanya kuwa na uelewa wa ubunifu.. ila pale unapochukua ufundi kushona, ubunifu wa vitu nilivyovitaja hapo na kuvifanya mtaji wa biashara
Ndo vinakufanya kusimama kama mbunifu wa mavazi… kipaji chako kinageuka kuwa ajira
Kwa kuzingatia hilo mafundi wengi wanalewa sifa kwakuwa wanauwezo wa kunakili kazi za wabunifu na wao wanajiona ni wabunifu.. sidhani kama ni kosa au wanapaswa kubezwa.. ningependekeza wawekezaji wakaona fursa kwa mafundi hawa kukusanywa na kuwezeshwa hata kwa viwanda vidogo kuweza kuboresha kazi na kuziuza kwa bei nzuri ili industry yetu ikue..
Sitegemei kama ni vyema kudiscuss about hakuna wabunifu, kuna mafundi cherehani kama ni suluhisho ila maswali yetu yawe wanafocus upande wa pili wa shilingi kuweza kuwasaidia hawa mafundi chelehani zaidi kukua
Afroswagga: Je vipi kuhusu kuigiana kazi?
2. Wabunifu kuigana kazi..? Sidhani kama ni kuigana ila naona ni mawazo au fikra kuendana tu.. unapoitwa mbunifu tayari inaonesha una karama ndani yako ya kubuni ila pale mawazo yanapogongana na mawazo ya mbunifu mwingine hicho ni kitu kizuri maana uwezo wa kuboresha kilichobuniwa na malighafi zilizotumika ndo kunanogesha kazi
Najua kuigana kupo ila sidhani kama kunaathiri ila sana sana kunakufanya mbunifu kubuni vitu vigumu zaidi kuliko mwanzo ili usiibiwe ubunifu wako
Martin asante kwa muda wako tuna appreciate kwa kuchukua muda wako kutufumbua macho kuhusu swala hili. Ps: tuna subiri new collection
Related posts
1 Comment
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More Information here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/martin-kadinda-kwa-sasa-tanzania-hakuna-tofauti-ya-wabunifu-na-mafundi-cherehani/ […]