Kuna msemo unasema miluzi mingi ina mpoteza mbwa, yes hii ni kweli kabisa na sio tu katika maisha bali katika mitindo na urembo pia.
Unaweza kukuta aina fulani ya vazi au urembo unakuwa hyped na fashionista’s, Influencers etc na wewe ukaona ununue uvae.
Sio mbaya ku keep up na fashion lakini kabla ya kufanya maamuzi ya kununua kitu hiko Jiulize maswali haya manne
1) Je Inasupport Aina Ya Mwili Wako?
Sote tuna support body positivity lakini kuna vitu mtu wa mwili wa aina fulani akivaa anaweza kushangaza wengine, sio kila kitu kinaweza kuvaliwa na kila mtu.
Unaweza kununua hiko kitu kwa bei ghali na usikivae sababu ukaona hupendezi
Ukakivaa lakini usiwe comfortable nacho hakikisha trend inayoendelea inafaa mwili wako.
DondooJua Aina Ya Mwili Wako Na Mavazi Yanayo Kufaa
2) Je ina compliment style yako?
Hii pia ni muhimu mfano wewe ni mtu wa viatu vifupi unaona trend ya highheels kila mtu anavaa basi na wewe unakimbilia kununua matokeo yake viatu vinaishia kuchubuka kwenye shoe rack huvivai. Hakikisha kabla hujarukia trend iwe ina compliment style yako ya kila siku.
3) Je ni kweli umekipenda?
Kama tulivyosema mwanzo miluzi mingi humpoteza mbwa, inawezekana hata hio trend hujaipenda ni vile tu kila unapopita unakutana nayo mwishoe unaamua tu na wewe uwe nacho na matokeo yake kuishia kukaa kabati bila kuvaliwa
4) Je Utakivaa Hata Baada Ya Trend Kuisha?
Some trend zipo timeless zinaweza kuvalika hata baada ya ile hype kuisha na kuna nyingine ni za muda tu. Ambapo ikiisha muda wake ukija kuvaa unaonekana wa zamani unachoyakiwa kufanya ni kununua zile ambazo unaona hata mara baada ya trend kuisha unaweza kuzitumia tena
Well ni matumaini yetu tumeweza kukusaidia kwa namna moja au nyingine tuambie ni trend gani uliirukia na sasa huwezi kuvaa tena?
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on to that Topic: afroswagga.com/mitindo/maswali-ya-kujiuliza-kabla-hujanunua-kitu-kinacho-trend/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/maswali-ya-kujiuliza-kabla-hujanunua-kitu-kinacho-trend/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/maswali-ya-kujiuliza-kabla-hujanunua-kitu-kinacho-trend/ […]