Kuvaa mavazi / nguo ambazo zinaachia wakati wa usiku ni muhimu hasa katika mzunguko wa damu lakini pia kuifanya ngozi ipumue, kuvaa mavazi yanayo bana kama tight, mavazi yenye elastic kiunoni au tops za kubana zinaathiri mzunguko wako wa damu na kutatiza uwezo wako wa kupumua kawaida, na kunaweza pia kusababisha muwasho wa ngozi.
Vitu gani unatakiwa kufanya?
- Usivae Brazia
Kuna uvumi wa kwamba unapolala na brazia basi inazuia maziwa kulala siku zijazo, lakini huu uvumi ni potofu, unapo lala ukiwa umevali brazia unaweza kujisababishia matatizo mbalimbali ikiwepo kuzuia mzunguko wa damu, kusababisha matatizo ya kutokupumua vyema lakini pia unaweza kupata fangasi hasa kwa wale tunaoishi maeneo yenye joto, na hii inatokea pia kwa wale ambao tunaopenda kulala na nguo za chini za kubana.
- Vaa Mavazi / Nguo Zisizo Bana
Utafiti unaonyesha kuwa kuvaa nguo za kubana usiku kunaweza pia kuzuia utengenezaji wa melatonin ambayo inawajibika kudhibiti mzunguko wako wa usingizi, na ikiwa circadian rhythm mwili wako hauko sawa, basi hii inaweza kuathiri ubora wa usingizi wako.
- Vaa Mavazi Ya Cotton (Pamba)
Pamba ndio material bora kabisa ya kulalia, inafaa kwa sababu ni nyuzi asilia ambayo ni nyepesi, laini na comfortable, zaidi ya hayo, inaruhusu ngozi yako kupumua na kuna uwezekano mdogo sana wa kusababisha mwasho wa ngozi au vipele, haswa ikiwa nguo haikubani Ikiwa pamba sio kwako, basi vitambaa vingine kama vile hariri au kitambaa cha mianzi (bamboo fabric) ni mbadala mzuri.
Well tuambie huwa unalala na mavazi ya aina gani?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…