Linda Bezuidenhout linaweza kuwa jina geni kwa wengi lakini kama ni mfuatiliaji wa mitindo huwezi kukosa kumjua, Linda ni chotara wa ki Tanzania na Dutch ni mbunifu ambae yupo katika ulimwengu wa mitindo kwa miaka 20 sasa. Linda kwa sasa anaishi Atlanta, ambapo bado anaendelea na kufanya ubunifu.
hivi karibuniLinda na kampuni yake ya LBC (Linda Bezuidenhout Couture) imefanikiwa kumvalisha mke wa Rapper T.I, Tiny Harris katika jarida la upscalemagazine 2017 Holidays issue.
Tumepata kuongea nae mawili matatu kuhusu kupata deal hii ambayo ni kubwa
Afroswagga – tungependa kujua ilikuaje mpaka ukaweza kumvalisha Tiny?
Linda – Mimi ni Designer mkubwa hapa Atlanta mastar wengi wanatambua kazi zangu Alhamdulilah.
Kwahiyo walivotaka nguo ya couture na walitaka iwe ya Designer wa hapa hapa Atlanta wakurugenzi wa upscale magazine wakaja Linda Bezuidenhout Couture Boutique ndo wakaja dukani. Wakachagua nguo 3 Kati ya zile 3 hiyo ndo ilipendwa zaidi Tiny.
Afroswagga – baada ya kumvalisha deals zimeongezeka?
Linda – Ofcourse kumvisha mtu maarufu kama Tiny inatangaza brand yetu kwa kasi sana na kuongeza wateja Alhamdulilah
Kwa upande wa deals hizo uwa zina kuja kwa ghafla uwa ni mipango ya mungu na sio kwa ajili ya kumvalisha Star Alhamdulilah 🙏🏾
Afroswagga – Je unaplans za kufungua Linda Bezuidenhout Tanzania?
Linda – InshaAllah ntaanza na consignment store kwanza kujaribu soko. Yani ntafanya mkataba na Boutique yenye Adhi kubwa ili iweke LB dukani mwao na kawaida ya Consignment business mwenye duka atachukua asilimia 40 kwenye kila gauni litakalo uzwa. Tukiona soko zuri basi tutafungua brunch ya LB Tanzania InshaAllah
Yani mwenye duka hato nunua LB ntampa tu aweke dukani itakapo uzwa tutagawana mauzo wao watachukua 40% MIMI 60%
Kwa wenye maduka makubwa Linda ana wapokea kwa mikono miwili, sisi kwetu tunasema hongera Linda na endelea kupeperusha bendera ya Tanzania kupitia ubunifu wako.
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/mitindo/mbunifu-linda-bezuidenhout-ametuambia-ilikuaje-kumvalisha-mke-wa-rapper-t-i/ […]
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/mbunifu-linda-bezuidenhout-ametuambia-ilikuaje-kumvalisha-mke-wa-rapper-t-i/ […]