Kwetu sisi ukiongelea mbunifu wa mavazi ya kiume ambae anahitaji kila aina ya heshima basi una muongelea Sheria Ngowi, Sheria is a legend & he will surely leave a legacy siku moja. Kuna ambao hamumjui Sheria ni nani labda kwa sababu tu kwa sababu ana fanya kazi yake iongee zaidi kuliko yeye mwenyewe, si mtu wa kiki havalishi models wanaojulikana mavazi yake ili kupata kiki. Tunaweza kusema Sheria ni kama Kobbe yupo slow but sure.
Wengine tunamjua kwa jina la Sheria Ngowi lakini jina lake halisi ni Walter Thomas Ngowi, Sheria Ngowi ni brand name yake ambayo yeye ameikuza kupita jina lake na sio kutaka umaarufu wa yeye mwenyewe kuliko brand yake, kama ambayo tulisema katika vitu vya kuzingatia ili kuacha legacy katika tasnia hii ya mitindo kimoja wapo ni kukuza jina la bidhaa yako kuliko kutaka kujulikana wewe mwenyewe kuliko kazi yako.
Sheria kwa sasa ameshavuka kuitwa mbunifu wa kitaifa bali ni mbunifu wa kimataifa kwanini? Sheria ana show case collection zake nje ya Nchi na zinapokelewa vyema, ana unique taste katika bidhaa yake. Kitu ambacho utakiona kwa Sheria ni aghalabu kukiona kwa mtu mwingine tukiongelea materials na finishing za kazi yake.
Japokuwa hapa kwetu haongelewi sana lakini Sheria anaongelewa na magazeti makubwa ya mitindo Nje ya Nchi, gazti kubwa la mitindo GQ Italia walishawahi kufanya nae interview na kumuweka katika Gazeti lao, ilikuwa mwaka 2011 ana miaka mitatu toka anaanze kuwa mbunifu, na kuweza kutamuliwa na gazeti kubwa kama hilo ambapo tunaweza kusema ni moja kati ya wabunifu wachache kutoka Africa Mashariki waliopata nafashi hio.
Tuzo! Tuzo! Tuzo! wanasema nabii hakubaliki kwao, au labda hapa kwetu ushindani ni mkubwa kuliko Nchi nyingine hatuwezi kuhesabu Sheria amepata tuzo ngapi ndani na Nje ya Nchi lakini ambayo ameipata hivi karibuni ni ya Mbunifu Wa Mwaka Africa – 2017 katika tamasha la Abryanz Style & Fashion Awards ambazo hufanyika huko Uganda. Na alishindanishwa na wabunifu mbalimbali kutoka Nchi mbalimbali kutoka Africa lakini alifanikiwa kuchukua yeye mbunifu kutoka Tanzania.
But then Sheria is No Avarage Guy, ana wavalisha ma – Rais kutoka Nchi mbalimbali za Africa na wabunge.
Tanzania needs to celebrate Sheria Ngowi, anafanya mambo makubwa na hajitangazi tu yeye bali ana tangaza Nchi nzima, anapo enda kuonyesha collection yake ya mavazi Nchi kama South Africa au London anaenda kama Sheria Ngowi mbunifu kutoka Tanzania, kama akifanya vizuri inamaanisha watataka kumjua na kujua Tanzania kunanini? ikiwa katika ulimwengu wa mitindo na vingine kwa ujumla.
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/mitindo/mbunifu-sheria-ngowi-ni-mfano-mzuri-wa-msemo-nabii-hakubaliki-kwao/ […]