Tuliwahi kuongelea kuhusu unisex fashion na namna ambavyo wabunifu wanavyo buni mavazi ya aina hii kwa kasi, Unisex fashion and style ni mavazi yanayobuniwa na kuweza kuvaliwa na jinsia zote yaani ya wanaume na wanawake. Hii ni kwa mashati, sketi, suruali na hata accessories za mwilini.
Kwa sasa tunaona style hii ikiwa inaingia Tanzania taratibu, ikiwa ni wabunifu kubuni mavazi ya aina hii lakini pia tumeona watu maarufu mbali mbali wakiwa wanavalia mavazi na accessories za namna hii, kwa upande wa kike ilichukua muda kuona wanawake wakiwa wanavaa suruali Africa au hata hapa Nchini kwetu ilikuwa inaitwa uhuni, lakini taratibu ikakubalika na kwa sasa wanawake wanavaa suruali kama ambavyo wanauwe wanavaa bila kuwa judged.
Inaonekana shilingi inataka kugeukiwa kwa wanaume nao kuanza kuvaa mavazi na accessories ambazo zinaaminika za kike, tumeona watu maarufu mbalimbali wakiwa wamebeba mikoba ya kike, kuvaa vikuku lakini pia hata kubeba mikoba,kwa hapa kwetu Tanzania tumeona watu maarufu kama Diamond Platnumz akiwa amevalia kikuku, alipata backlash kubwa sana lakini ilionekana sio yeye tu Duniani ambae amevaa kikuku, watu kama Chris Brown na Dwayne Wade nao walishawahi kuvaa
Wakati tukiwa tunamuongelea Diamond, tukamuona mwanamitindo Calisah ambae yeye alikuwa kazini na akavaa viatu vya kike katika kutangaza duka hilo la viatu na alipo ulizwa alijibu kwa kusema kama akilipwa vizuri hata gauni anaweza kuvaa yupo kazini, na yeye pia alipokea backlash kubwa kutoka kwa watu mbalimbali lakini pia na yeye si mwanaume wa kwanza kuvaa heels Duniani watu maarufu mbali mbali na hata models wakiume kutoka Nchi za wenzetu huvaa viatu hivi, akiwepo mbunifu na Rapper Kanye West.
Wakati juzi tumemuona msanii anaye chipukia Twaha Mabantu, yeye aliamua kuvaa gauni kabisa amemalizia na viatu na socks,hii ikatufanya tu-notice kwamba kama ambavyo wanawake waliweza taratibu kuvaa mavazi ya kiume basi ndivyo ambavyo mtindo wa wanaume kuvaa mavazi ya kike na urembo wa kike unavyo anza kukua taratibu na inawezekana ikafika kipindi tukawa tunavaliana mavazi bila ya watu kushangaa wala kutoa backlash
Well afromates je mtaikubali hii style ya wanaume kuvaa mavazi ya kike kama ambavyo wanawake wanavaa mavazi ya kiume?
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you will find 22104 additional Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/mitindo-ya-unisex-inavyokuja-taratibu-nchini-tanzania-20669/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 77796 additional Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/mitindo-ya-unisex-inavyokuja-taratibu-nchini-tanzania-20669/ […]