Ni jumatatu nyingine ambayo watu wengi wana pata shida kuchagua nini wavae ofisini, ukizingatia ni mwezi mtukufu huwezi kuvaa suti ya sketi fupi au suruali ya kubana, inachukua muda kupata suluhisho hasa kwa upande wa wadada lakini tusicho jua kuna vitu vichache tu ambavyo vinaweza kutusaidia kupata muonekano wa kiofisi ukiwa umejistiri
- Koti
Hakikisha katika kabati lako hukosi makoti ya mikono mirefu yenye rangi tofauti tofauti, lakini hizo rangi zinategemea na mazingira ya ofisi yako kama hayaruhusu basi usivae rangi zinazo ng’aa sana vaa nyeupe,nyeusi,udongo au kijivu kama mazingira yana ruhusu basi una weza kuvaa njano,nyekunde kijani nk. Koti linakupa muonekano wa kiofisi Zaidi
- Suruali isiyo bana
Kitu kizuri kuhusu suruali zisizo bana ni kwamba zinatengenezwa kimitindo na pia unakua upo huru, ukitaka kuwa kawaida vaa nyeusi,udongo au kijivu hizi zimetulia na utaonekana mtu makini kabisa anae jua nini anafanya, lakini ukitaka kuonekana Zaidi vaa rangi ya kaki.
- Maxi sketi
Maxi sketi ni chaguo lingingine ambalo haliwezi kukuangusha ukivaa ofisini, ukizivaa vizuri unapendeza na zinakupa muonekano wa kifahari, ndefu na hazibani achana na matirio ya kitambaa kuwa makini katika kuchagua rangi nyeusi, kijani, rangi ya chungwa nk vaa na blauze nzuri na mkanda wa tumboni itapendeza Zaidi.
- Hijabi
Vaa hijabu yako uki yakinisha na rangi moja ya katika vitu ulivyo vaa kama rangi ya sketi na hijab au rangi ya blauzi na hijab.
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…