Kama tunavyojua Y2K fashion imerudi, style nyingi ambazo zilikuwa zinatumika miaka ya zamani zinaonekana kurudi kwa kasi na kwasasa kubwa tunayoiona ni cargo pants. Kama hujui Cargo Pants ni nini ni zile suruali ambazo zinakuwa na mamifuko makubwa na mara nyingi huwa zinakitambaa kigumu japo kwasasa zimetoka za material mbalimbali.
Inawezekana unayo na hujui ui-style vipi au unajua na namna ya kui-style ila ungependa kupata namna nyingine nyingi za ku-style vazi hili basi tupo hapa kwaajili yako.
Na Tshirt / Top
Inategemea na uendapo na mapenzi yako kama huna mtoko wa maana unaweza kuvaa na simple sandals au kicks lakini kama una mtoko basi unaweza kuvalia suruali hizi na heels kama Kim Kardashian hapo chini

Cargo Pants Na Crop top
kuna wale tunapenda kuonyesha matumbo au kuwa stylish kwa kuvaa crop top unaweza ku-style cargo pant yako na crop top, unaweza kuongezea na jacket juu au hivi hivi na kupendeza.

Cargo Pant Na Body Suit
Cargo pant inaweza kuvaka na body suit, uka istyle kutokana na mazingira uliyopo au unayokwenda, unaweza kuvaa off shoulder bodysuit, spaghetti strap body suit au hata body suit ya mikono mirefu ni wewe na comfortability yako.

Cargo pants zinaweza kuvaliwa na chochote iwe kuanzia shirts, vest’s, corset top’s na nyinginezo lakini pia zinaweza kuvaliwa na boots ziwe ndefu au fupi, raba, heels etc. Na unaweza kuvaa kwenye mitoko ya usiku, date, casual wear na hata kwenda brunch na marafiki. Well hizi ni chache ambazo tumeweka lakini zipo namna nyingi nyinginezo unazoweza ku-style vazi hili, muhimu ni kujua namna ya kucheza nalo.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…