Moja kati ya vitu ambavyo wengi tunapitia ma-ofisini ni kuwa confused kati ya kuwa over dress na ku-low dress ofisini na chaguo kubwa huwa kuwa katikati yaani usiwe low wala over dressed na hapa ndipo tunapokutana wengi unakuwa na ma shirt yako ya rangi moja kadhaa, skirt kadhaa na suruali ukamalizia na handbag yako na viatu basi mwisho wa siku ofisi nzima tunafanana kasoro rangi za nguo tu lakini ni namna gani unaweza kuwa stylish ofisini?
Toka Kwenye Plain Clothes Na Anza Kuvaa Pattern
Wengi ofisini tunavaa plain clothes utakuta umevaa plain white shirt na plain black trouser au skirt, toka hapo na anza kuvaa zenye pattern kama top plain basi chini valia suruali/skirt ya pattern na kama skirt / suruali plain valia top yenye pattern hakikisha rangi zinaendana

Vaa Mavazi Ya Rangi
Hakuna sehemu imeandikwa rangi za mavazi ya kazini yawe black, white, au blue tu jamani kuna colors nyingi ambazo zina pop lakini zimetulia vyema tu unaweza kuvaa ofisini kama maroon, emerald green, mustard yellow etc lakini pia hakikisha hazipigi kelele sana na kama utavaa juu rangi ina pop chini vaa calm color

Pop Color Na Viatu / Handbag
Kama sio mpenzi wa mavazi ya rangi rangi basi kati ya viatu au handbag hakikisha ina rangi ya kuvutia ambayo itafanya wengine wageuze shingo kukuangalia wewe

Accessorize
Miwani sio mpaka uwe unaumwa macho jamaniunaweza kuvaa tu kama accessory kuna miwani ambayo ni kama ya macho lakini ni ya urembo unaweza kuchagua unayoona inakufaa ukavaa, vaa belt pale vazi lako ninapohitaji mfano unavaa black little dress unaweza kuongezea na animal print waist belt, pochi pia inaweza kuwa namna nzuri ya kuongezea udambwi kwenye vazi lako la ofisini

Well Tukutakie Slayage Njema Week Hii
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-5-za-kuonekana-stylish-kazini/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-5-za-kuonekana-stylish-kazini/ […]