Kuna nguo zinaendana na kila kitu. Yani hizi nguo ukinunua ni kama vile umewekeza..hautajuta. Kwanzia kwenye good days hadi zile siku hutaki kusikia suala la kuvaa, basi hizi nguo uwa tayari kuvaliwa. Tshirt ni miongoni mwa hizi nguo. Unaweza kuvaa tshirt na kitu chochote hususani ikiwa plain lakini ni namna gani unaweza ivaa ukatokea kipekee zaidi? Niko hapa kukueleza namna unaweza style tshirt yako kama ifuatavyo. Usisahau style ni uhuru kuwa uhuru kufanya majaribio na nguo zako unaweza pata muonekano nadhifu zaidi.
Imeandikwa na @style.with.mimie
T Shirt , sketi na raba
Huu muonekane uwa casula ila ni casual kali hatari. Unaweza vaa sketi ndefu inayobana, sketi fupi au inayofika chini kidogo ya magoti. Ni vizuri zaidi ukichomekea au ukiifunga shati kwa mbele kama umevaa sketi ya high waist au unataka tu kuachia ngozi kidogo. Aina ya viatu unavyovaa vinakamilisha muonekano. Unaweza kuongezea accessories simple ili kutunza muonekane wako, too many accessories zinaweza haribu the whole look.
Shati, jeans na kiatu kirefu
Wale wanaopenda smart casual looks, hii ni yenu. Kuna jeans za kila aina; sketi, suruali, pensi, mini skirt, overrall, yani kila aina. Imagine umetupia shati plain na zile suruali ambazo chini zimechanwa, kiatu kirefu na handbag kali. Umeona hatari inayotokea hapo? So muhimu ni kiatu kizuri. Unaweza vaa mkanda pia ili kuongeza vionjo.
Shati,koti na kofia
Ni muhimu kutoka kitofauti, watu wengi hawajazoea kuvaa kofia na koti ila this is a look. Unapoongeza accessories keep it simple na kama unavaa statement piece basi jitahidi iwe moja tu. Hakikisha unapangilia rangi zako vizuri na koti lako liwe zuri linaloendana na mavazi yako mengine na liwe linaendana na mwili wako.
Shati na kofia ya duara
Watu wachache wana ujasiri wa kuvaa hizi kofia, nataka na wewe uwe miongoni mwa hawa watu. Ukiwa na nguo yako iwe ni suruali, sketi, kaptula..n.k basi unaweza ivaa na shati na kofia ya duara. Shati unaweza kuifunga au unaweza chomekea. Unaweza vaa na high heels zilizo wazi, buti, flats au raba.
Shati kubwa na mkanda mnene au kiatu matata
Huu ni muonekano wa tofauti na unafaa zaidi mitoko na washkaji, sehemu za starehe na sehemu zote ambazo kuvaa nguo fupi sana sio ishu. So kama una shati lako, ni kubwa sana..unaweza livaa na boots zinaweza kuwa ni ankle boots au buti ndefu hadi magotin. Pia unaweza vaa na raba au kiatu kirefu chochotei. Bana shati kwa mkanda mnene au kufunga sweta kiunoni. Unaweza vaa na kofia au kuweka cheni. Cheza na mavazi yako.
Shati na kitenge
Kitenge ni vazi flani lenye rangi nyingi, ukivaa na shati plain basi unabalance mambo. Unaweza vaa na nguo yoyote ya chini ya kitenge na kunogesha muonekano kwa accessories mbalimbali. Hakikisha viatu vinaendana na muonekano wote.
Shati na suti
Kama unataka kupunguza makali ya suti a.k.a “tone down” basi vaa tshirt ndani ya suti. Hii itasaidia suti ionekane casual zaidi. Ukitaka kuwa casual zaidi basi ongeza na raba miguuni na vaa accessories chache sana, ikibidi usivae. Pia usivae rangi nyingi sana. Jaribu kumechi rangi ya shati na viatu au shati na mkoba.
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you will find 89580 more Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-7-za-kipekee-za-kustyle-t-shirt/ […]
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-7-za-kipekee-za-kustyle-t-shirt/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-7-za-kipekee-za-kustyle-t-shirt/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-7-za-kipekee-za-kustyle-t-shirt/ […]