Tumeingia kumi la pili katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, Week iliyopita tuliona jinsi ambavyo watu maarufu mbalimbali wali-style mavazi yao wakati wamekwenda kufturu pamoja na kuzindua kipindi cha nyumba ya Imani katika wasafi headquater,
Well week hii tunaangalia watu maarufu mbalimbali walivyo style vazi la kanzu
Tuaze na Bdozen mtangazaji kutoka Clouds Fm, yeye alivalia Kanzu nyeupe, ameistyle na eghal ya rangi nyekundu na nyeupe amemalizia muonekano wake na miwani na kobazi na socks, he looks dapper as he always does.
Tunakuja kwa mwanamuziki Fid Q au Fareed Kubanda yeye aliamua kuvaa kanzu ya rangi ya blue ( ni mara chache kuona mtu amevaa kanzu ya rangi rangi), Kanzu hii ina urembo mweupe amemalizia muonekano wake na suruali nyeupe, eghal yenye rangi nyeusi na nyeupe na viatu vyenye rangi iliyo endana na kanzu. Fid looks good hapa unaweza kuona amefanya effort katika hili vazi, but well Fid fanyia utaratibu hizo ndevu basi hata kitana tu kipite all in all amependeza.
Gabo yeye ni kama ameupania hivi huu mwezi maana kila post amependeza hadi kazi kuchagua ipi tumeipenda zaidi ya ipi, leo tuna share nanyi outfit zake mbili kati ya nyingi alizopost ya kwanza hii ambayo aliamua kuvaa all white, kanzu nyeupe, eghal nyeupe, viatu vyeupe amemalizia muonekano wake na miwani, saa na kifimbo you can never go wrong in white.
Hapa ilikuwa same outfit sema akaongezea na hili dish-dash kwa nje, unaweza kuona jinsi ambavyo unaweza kuvaa vazi hili mara nyingi kwa kuongeza tu accessories mbalimbali.
Wa mwisho kwa leo tunamalizia na msanii Ommy Dimpoz ambaye na yeye alivaa all white kanzu nyeupe na turban nyeupe, amemalizia muonekano wake na miwani pia.
Well kama ambavyo unaona vilivyo inekana kuwa in common ni viremba, miwani na saa, kama ungependa kuvaa kanzu yako ionekane stylish basi ongezea hivyo vitu. Tuambie kwa upande wako nani kakuvutia zaidi kati ya hawa wanne?
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ambavyo-watu-maarufu-wame-style-kanzu-zao/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ambavyo-watu-maarufu-wame-style-kanzu-zao/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here on that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ambavyo-watu-maarufu-wame-style-kanzu-zao/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/mitindo/namna-ambavyo-watu-maarufu-wame-style-kanzu-zao/ […]