Fanny Packs zimekuwa kwenye trend kwa muda sasa ni vijipochi fulani vya kuvaa kiunoni, watu maarufu mbalimbali wameonekana wakiitumia trend hii, fashionista’s, stylist na wengine wengi. Lakini pia designers wakubwa kama gucci wameonekana kubuni vipochi hivi katika collection zao, hapa kwetu wasanii kama Dogo Janja,Juma Jux wameonekana kuvutiwa na trend hii pia.
Tunajua kwa sasa tuna Hijabista’s mbalimbali ambao wanatuonyesha namna ya kuwa modest huku ukiwa umejistiri na leo tumekuletea namna ambavyo hijabista mbali mbali wame jaribu kustyle trend hii huku wakiwa wamejistiri.
Hijabista Fatema yeye ameonyesha namna ya kustyle fanny pack na pleated skirt na turtle neck top, amemalizia muonekano wake na boots.
Wearing one color is so in right now hijabista huyu yeye amevaa wide leg pants za red, top ya red na funny pack ya rangi hio hio huku akimalizia muonekano wake na brown sandals na brown hijab.
Hijabista Mariam Mohammad yeye amevaa fanny pack yake nyeusi na long tuxedo dress/coat nyeusi na ruffle blouse nyeupe huku akimalizia muonekano wake na hijab nyeupe na long black heels.
Mariam tena akiwa amebeba fanny pack yake nyeusi huku akiwa amevalia all white assemble lakini mtoko huu ni casual zaidi.
Tuambie wewe ungestyle vipi fanny pack yako?
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…